Habari za hivi Punde

WAZAZI NA WALEZI WANASHINDWA KUCHANGIA MIRADI YA MAENDELEO.

.

BAADHI  ya wazazi  na walezi  manispaa ya Shinyanga  asilimia kubwa wamekuwa  hawapendi kuchangia miradi ya maendeleo  mbalimbali ikiwemo  sekta ya elimu  hali ambayo imeonyesha  katika shule ya sekondari Mazinge kushindwa kuchangia  huduma ya wanafunzi kupata uji na chakula cha mchana.

Ikiwa kila mwanafunzi  inatakiwa achangie kiasi cha shilingi 3000,  hivyo Idadi ya wanafunzi waliotoa michango yao ni 6 pekee kwa shule nzima kati ya  wanafunzi 664 kwa lengo la kupata uji  wawapo shuleni hapo, imeelezwa  wazazi ndio chanzo cha kudhorotesha  kutokupata huduma hiyo ikiwa katika sherehe za harusi wanakuwa mstari wa kwanza  kuchangia.

Diwani wa kata ya Ndembezi katika manispaa ya Shinyanga David Nkulila,ambaye pia ni naibu meya wa manispaa hiyo aliyasema hayo wakati wa kikao cha kamati ya maendeleo ya kata hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya afisa mtendaji wa kata hiyo.


Nkulila alisema hayo baada ya kupewa taarifa na mkuu wa shule ya sekondari Mazinge iliyopo katika kata hiyo,kuhusu mchango kwa ajili ya wanafunz 664,ambapo kati ya hao 6 pekee wamechanga huduma ya uji  tangu mwaka jana.

Nkulila alisema ni vyema sasa wananchi wakabadilika na kuona umuhimu wa kujali watoto kwamba tatizo siyo wananchi kukosa elimu bali kinachotakiwa ni wananchi kupewa hamasa na viongozi kuwa mstari wa mbele kuchangia.

“Wananchi  wanahitaji hamasa siyo elimu,na katika hili sisi viongozi tunapaswa kuwa wa kwanza kuchangia hata kama hatuna watoto katika shule,mimi nilichangia magunia ya mahindi katika shule za kata hii,na  nimetoa gunia la mchele katika shule ya sekondari  Mazinge”,aliongeza Nkulila.

Naye mkuu wa shule ya sekondari Mazinge Henry Ntuah alisema sababu zinazopelekea wananchi kuwa nyuma kuchangia elimu mfano huduma ya chakula kwa wanafunzi ni wazazi na walezi kutohudhuria vikao vya shule pindi wanapohitajika.

Ntuah alisema wazazi wanaohudhuria vikao vya shule ni wachache matokeo yake utekelezaji wa mpango wa chakula kwa wanafunzi ikiwa ni agizo la mkuu mkoa wa Shinyanga kwa kila shule kupata huduma ya chakula na uji unakwama.

Nao wajumbe wa kamati hiyo mbali na kumpongeza diwani wa kata hiyo kuwa mstari wa mbele kuchangia sekta ya elimu katika kata yake ,ambapo mratbu elimu kata Seleman Bulugu alisema kuwa  diwani aliweza kutoa  michango  ya  magunia kumi na moja kwaajili ya shule tatu za msingi zilizopo kwenye kata huku  wakitaka  viongozi wengine kuiga mfano wake.

0 Response to "WAZAZI NA WALEZI WANASHINDWA KUCHANGIA MIRADI YA MAENDELEO."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.