Habari za hivi Punde

MTOTO ALIYECHINJWA NA BABA YAKE NA KUTOKWA DAMU NYINGI SASA AFARIKI DUNIA

MTOTO   Said Joshua (12) aliyekatwa koromeo  kwa kutumia kisu na baba yake mzazi huko wilayani Kahama mkoani Shinyanga amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa ya Bugando jijini Mwanza.
 
Mtoto huyo ambaye alichinjwa na baba yake aitwaye Joshua Salvatory (37),fundi baiskeli akiwa nyumbani kwake usiku wa kuamkia tarehe 4 mwezi huu katika kitongoji cha Majengo Kaskazini,kata ya Majengo,tarafa ya Kahama mjini  mkoani Shinyanga amefariki dunia jana jioni  majira ya saa kumi kasorobo.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa Kitongoji cha Majengo Kaskazini Noel Makula Museven alisema mtoto huyo alifariki akiwa Bugando alikokuwa amelazwa kwa matibabu zaidi mara baada ya hali yake kuwa mbaya katika hospitali ya wilaya ya Kahama alikokuwa anapatiwa kutokana na koromeo lake kukatwa lote kwa kisu na baba yake kutokana na kile kilichodaiwa kuchoka kumtibu maradhi yaliyokuwa yanamsumbua mara kwa mara. 
 
Kitendo cha kuchinjwa kwa mtoto Said Joshua na hatimaye kusababisha kifo chake kimeibua mambo mengi huku baadhi ya wakazi wa Kahama wakidai kuwa pengine kitendo hicho kinatokana na imani za kishirikina kwa madai kuwa mtuhumiwa alikuwa amemtoa sadaka mwanae kwa waganga ili kupata utajiri.
 
Baadhi ya wananchi walisema Salvatory amefanya kitendo hicho kwa lengo la kulipa mchango wa Freemason na kwamba alitaka kuchangia damu ya mtoto mdogo akakataliwa.
 
 
“Ndugu mwandishi haya mauaji wengi wanayahusisha na imani za kishirikina kwani hivi sasa jamii ya wana Kahama inakabiliwa na balaa la kuamini vitu na mambo yasiyo na msingi kama lile la kubaini wachawi na imani ya Freemason ambayo haijulikani hata ilikotoka wala msingi wake”,alisema mkazi wa mmoja wa Kahama.
 
Naye  mwenyekiti wa  Kitongoji cha Majengo Kaskazini Noel Makula Museven alisema kifo cha mtoto huyo kinatokana na imani za kishirikina kwani kumekuwepo na taarifa kuwa  Joshua Salvatory alikuwa amemtoa sadaka mwanaye Said Joshua kwa waganga ili awe tajiri.
 
 
Museven alisema  kuwa akiwa bado yu tajiri Joshua Salvatory alikiuka masharti ya mganga wake pesa zikamwishia na mtoto wake akaendelea kubaki katika hali ya kuugua mara kwa mara ikiwemo kuanguka kifafa kila mwezi.
 
“Kitendo cha kufirisika kwa mtuhumiwa na mtoto kuendelea kuugua kifafa,nadhani ndicho kimemfanya ammalize tu mtoto huyu,taarifa za kwamba ana matatizo ya akili siyo kweli kwani mtuhumiwa kwanza na mwizi mzuri tu,amefikishwa polisi siku za nyuma kwa wizi,sasa inakuwaje mtu mwenye matatizo ya akili aibe?”,alieleza Museven.
 
 
Katika hatua nyingine Museven kabla ya kumkata koromeo mwanaye pia mwezi Julai mwaka jana Salvatory alitaka kumchinja mke wake Mariam Idd lakini yeye (Museven) akawasuruhisha na mke wa mtuhumiwa kuamua kumkimbia mme wake kwa hofu ya kuuawa na mwanamme kubaki na mtoto Said Joshua.
 
 “Haikuishia hapo siku chache tu mtuhumiwa pia alitaka kumchinja mtoto wa jirani yake kwa madai ya kwanini huwa anacheza na mwanaye ,kama mwenyekiti wa kitongoji nikaingilia kati kitendo hicho kilimuudhi Salvatory na kutaka kunichinja pia,nikaita polisi akakamatwa,na ndiyo tuhuma iliyompeleka gerezani kwa kipindi cha miezi miwili,na mtoto kurudi kwa mama yake”,alieeleza Museven.

Kwa mujibu wa mama mzazi wa mtoto huyo Mariamu Idd (35) alisema, mtoto wake alichukuliwa na baba yake mzazi siku moja kabla ya tukio na  kwenda naye kwake mitaa ya Majengo kwa kuwa  alikwisha achana na mwanamme huyo siku nyingi.

“Baba wa mtoto huyu siku za nyuma,alikuwa akimchukua mwanangu mara kwa mara na kumpeleka nyumbani kwake,mimi nilishaachana naye, huwa anamrudisha,na amekuwa akidai kuchoshwa na huduma za matibabu kutokana na mtoto huyo kuwa na matatizo ya kiafya”,alifafanua mama huyo.

 

0 Response to "MTOTO ALIYECHINJWA NA BABA YAKE NA KUTOKWA DAMU NYINGI SASA AFARIKI DUNIA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.