Habari za hivi Punde

MADIWANI HALMASHAURI MJI WA BARIADI WATAKA AGIZO LA RAIS KUTEKELEZWA HOSPITALI YA WILAYA KUWA YA MKOA



MADIWANI  wa Halmshauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu wamemtaka Mkuu wa Mkoa huo, Paschal Mabiti kutekeleza agizo la Raisi Jakaya Kikwete alilotoa wakati wa ziara yake mkoani hapa, la kupandisha kiwango hospitali ya Wilaya ya Bariadi kuwa hospitali ya Mkoa.

Mbali na Mkuu huyo wa Mkoa kutakiwa  kuhakikisha anatekeleza agizo hilo la Rais , madiwani hao walishangazwa na kitendo cha Kiongozi huyo wakati wa kikao cha ushauri cha Mkoa kilichokaa hivi karibuni kukataa kutekeleza agizo hilo kwa madai kuwa  Rais  hakuagiza kupandishwa kiwango hospitali hiyo.
 

Akiongea wakati wa kufunga kikao cha Baraza la madiwani wa halmashauri hiyo kilichofanyika jana mjini hapa, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Robert Lweyo, alimtaka Mkurugenzi Erika Msika kuandika barua kwenda kwa mkuu wa mkoa ya mkutaka kutekeleza agizo hilo.

Alisema kuwa wakati wa majumuhisho ya ziara ya Rais Mkoani hapa katika wilaya ya Busega, uongozi wa mkoa uliagizwa kufanya utaratibu wa kuhakikisha hospitali hiyo inapandishwa kiwango na kuwa hospitali ya mkoa kutokana  kwa sasa kukabiliwa na msongamano wa wagonjwa.

Alisema kuwa mara baada ya mkoa wa simiyu kuanzishwa, na makao makuu yake kuletwa wilayani bariadi, Hospitali hiyo imekuwa ikitumiwa na watu wengi kutoka katika kila wilaya kuleta wagonjwa wao kutokana na kuitwa hospitali ya mkoa.


“Raisi Kikwete aligiza kupandishwa kwa hospitali ya wilaya ya Bariadi, lakini Mkuu wa Mkoa amepinga agizo hilo, kwa kusema kuwa Raisi hakuagiza hivyo badala yake aliagiza Halmashauri hiyo isaidiwe na uongozi wa Mkoa katika kuongeza watumishi, pamoja na madawa ikiwemo fedha za matumizi kutokana na Halmashauri hiyo kuelemewa na wingi wa wagonjwa”alisema Lweyo.

Alibainisha kuwa uamuzi wa mkuu wa mkoa siyo sahihi, na Rais hakuagiza hivyo, ambapo walimtaka kurejea hotuba ya Rais wakati wa majumuisho yake  kwenye ziara yake mkoani hapa kwa kile alichokiongea juu ya hospitali hiyo.

Alisema azimio la Baraza hilo juu ya suala hilo limemtaka Mkurugenzi kuiandikia  barua ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuitaka kurejea hutuba ya Rais, ikiwa kuhakikisha agizo hilo la kiongozi wan chi linatekelezwa ipasavyo.
.



0 Response to "MADIWANI HALMASHAURI MJI WA BARIADI WATAKA AGIZO LA RAIS KUTEKELEZWA HOSPITALI YA WILAYA KUWA YA MKOA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.