Habari za hivi Punde

WADAU WA ELIMU WATAKA MFUMO UBADILISHWE ILI KUWEPO NA ULINGANO KWA WAZAZI





WAMILIKI na  mameneja  wa shule za msingi,sekodandari na vyuo binafsi   kutoka mikoa nane ya nchini Tanzania   wameitaka serikali  kubadilisha  mfumo  wa elimu  kutokana  na  wazazi wanaosomesha watoto wao  kukosa msaada  wowote  unaopelekea kutozwa   kodi  mbalimbali  zenye kiwango kikubwa.

   Hayo yalisemwa  na   mwenyekiti wa Tamongsco  Jerrry Nyabululu   kwenye mkutano wa wamiliki na mameneja  wa vyuo na shule zisizokuwa za serikali kanda ya Magharibi,kanda ya ziwa na kanda ya ziwa magharibi  kwa mikoa ya Kagera,Mara,Mwanza ,Simiyu,Geita ,Kigoma,Tabora na Shinyanga  katika  risala yao mbele ya mgeni rasmi ambaye ni  mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Rufunga akiwa ameambatana  na Hadija Mcheka  mkurugenzi msaidizi wa usajili  kutoka wizara ya elimu.

Hata hivyo  waliiomba serikali ianzishe mjadala wa kitaifa miongoni mwa wadau wa elimu ili ikiwezekana mfumo wa elimu ubadilishwe  kwani imeonekana kuwa mtoto ambaye anasoma shule  binafis hapati msaada wowote  kutoka  serikalini kwa kutozwa kodi  nyingi  kwa kiwango kikubwa  ikiwa wazazi wao ni walipaji wakubwa wa kodi  mbalimbali za serikali kama wazazi wengine wanaosomesha  shule  zingine.


Nyabululu alisema  kuwa mfumo huo ukiendelea  hapo badaye kutajengeka  chuki  na matabaka  yasiyo ya lazima  katika nchi, pia katika  suala hili la kodi ndio linalowaongezea gharama  za ada pia kuwa kubwa  wazazi wanaosomesha  watoto wao kwenye shule binafsi  hivyo wanaiomba serikali kuangalia upya sheria hiyo.

“ changamoto  zilziopo katika shule binafsi  kumekuwepo na  upandishiwaji wa riba kubwa wanapoomba mikopo kwenye taasisi za kifedha  kwa kufananishwa na wafanyabishara wakati wao wanachangia suala la elimu na kuwapatia vijana ajira ,ambapo kwa kanda  hizi tatu zilizopo  mafanikio ya baadhi ya shule zikiwemo Rockeni Hili ya wilayani Kahama na Kwema  zimefanya  vizuri  kwa kuongoza kitaifa  katika matokea yao kwa darasa la saba mwaka jana”alisema Nyabululu.

Mkurugenzi wa  shule ya  msingi na sekondari Kwema Pauline Mathayo aliyehudhuria mkutano huo alisema kuwa  matarajio wanayoyakusudia ni kuwepo kwa uchocheo mzuri kwa shule binafsi  ambao utawapa fursa ili kuendeleza kiwango cha elimu, ada zinazotozwa sio kubwa  kwa sababu  inaonekana hivyo kwa kutopata ruzuku kutoka serikalini,pia shule hizo zimeipunguzia serikali mzigo  kwa kutoa ajira kwa vijana.

Naye  mwakilishi   kutoka wizara ya elimu  kwa niaba ya kamishina wa wizara hiyo  Mcheka alisema kuwa   wizara sasa inampango wa uendeshaji wa shughuli za kiserikali kwa uwazi ambapo italenga   kwenye sera ya elimu ya mwaka  1995  kwa kufanyiwa marekebisho  ili kuweza kuendana  na usawa   kwa kuondoa changamoto hizo huku serikali bado inatambua mchango wao wa kuchangia kuondoa umasikini.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa shinyanga Ally Rufunga alisema kuwa  shule hizo zimekuwa zikitegemea walimu wastaafu na wale wa kutoka nje huku wakiwaacha vijana  wenye sifa nao wanaweza, pia tozo la kodi nyingi na kubwa  hiyo iangaliwe upya na wizara husika huko ni kumkandamiza mzazi wengine wanashindwa kupeleka watoto wao katika shule hizo kutokana na kiwango cha ada  kinacho tozwa ni kikubwa.

Alisema sekta ya elimu ilitoa fursa kwa  watu binasfi kutoa elimu   ambapo wamekuwa wakijitahidi kunyanyua kiwango cha elimu nchini hasa kwa mkoa wa shinyanga ambao ulikuwa ukishika nafasi ya mwisho kitaifa kwa  miaka mitatu mfululuzo huko nyuma  mpaka kufikia 2012  ikishika nafasi ya 13 kutoka ya 21 kwa kusaidiwa na shule binafsi kuongoza kitaifa ndani ya mkoa.

0 Response to "WADAU WA ELIMU WATAKA MFUMO UBADILISHWE ILI KUWEPO NA ULINGANO KWA WAZAZI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.