Habari za hivi Punde

ASUSIA KUISHI KWA KUJINYONGA HUKU AKIACHA UJUMBE MZITO- CHALINZE

ASUSIA KUISHI KWA KUJINYONGA HUKU AKIACHA UJUMBE MZITO- CHALINZE

shambani

Mwanamme mmoja ambaye hakujulikana jina, amekutwa akiwa amejinyonga ndani ya kibanda shambani huku akiwa na karatasi iliyoandikwa ujumbe “Nawaachia dunia yenu muishi miaka 110”


Mwenyekiti wa Kijiji cha Kibiki, Ally Hussein alisema  mwanamume  huyo amekutwa saa mbili usiku akiwa amefariki na hivyo kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi Chalinze.

Alisema askari walifika na kuukuta mwili wa marehemu ukiwa umefungwa kamba ya katani na alipopekuliwa alikutwa mfukoni na karatasi yenye maandishi hayo.

Kaimu Kamanda wa Polisi Pwani, Mrakibu msaidizi, Athumani Mwambalaswa amethibitisha tukio hilo na kusema mwili wa marehemu ulichukuliwa na kuifadhiwa Kituo cha Afya Chalinze kusubiri uchunguzi wa daktari.


Hata hivyo, alisema bado haijafahamika mtu huyo ni mwenyeji wa kijiji kipi kwani hapo Kibiki hakuweza kutambulika na jitihada za kutafuta ndugu zake katika vijiji vya jirani zinafanyika. Chanzo cha kujinyonga bado hakijajulikana.

NI KWELI MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YANAWEZA KUTOWEKA KUFIKIA MWAKA 2030?

DAWA  ZITASAIDIA KUONDOA CHANGAMOTO YA MAAMBUKIZI?


IMEELEZWA kwamba ifikapo mwaka 2030, kuna uwezekano mkubwa wa kudhibitiwa kwa  Janga la Ukimwi duniani,hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la Umoja wa mataifa la kupambana na Ukimwi.

Shirika hilo linasema idadi ya maambukizi mapya na wanaokufa
kutokana na Ukimwi imeendelea kushuka.

Hata hivyo jitihada zaidi za kimataifa zinahitajika kwani zilizopo hazitoshi kumaliza janga hilo.


shirika la misaada la Medecins Sans Frontieres limeonya kuwa watu wanaoishi na virusi hivyo hawapati dawa za kutosha.


Ripoti hiyo inaonyesha kuwa watu milioni 35 duniani wanaishi na virusi vya Ukimwi.


Ripoti hiyo ilionyesha kuwa maambukizi mapya milioni 2.1 yalitokea mwaka 2013. Idadi hii iko chini kwa asilimia 38 ikilinganishwa na mwaka 2001.


Vifo kutokana na HIV pia vimepungua kwa asilimia 5 katika miaka mitatu iliyopita. Kwa sasa watu milioni 1.5 hufariki kutokana na ugonjwa huo kila mwaka.

WANAJESHI WAAHIDI KUWEKA ULINZI KITUO CHA KULELEA WATOTO WENYE ULEMAVU WA NGOZI.

Wanajeshi  wa kikosi cha 516 kambi ya kizumbi wakifanya usafi wa mazingira katika kituo cha Buhangija kinacholea watoto wasioona,walemavu wa viungo,wasiosikia na Albino.
Sehemu ya misaada iliyotolewa na kikosi cha 516 kambi ya Kizumbi.
Watoto wenye ulemavu wa ngozi Albino wakiwa katika eneo la kituo chao wanapolelewa.
Misaada iliyotolewa na kikosi hicho ni pamoja na kilo 50 za sukari,mafuta ya kupaka cartoni mbili,ndoo mbili za mafuta ya kupikia,kilo 25 za unga wa sembe ,majani ya chai,chumvi,sabuni za kufulia pamoja na mbuzi wawili.
Watoto wanaolelewa katika kituo cha Buhangija wakiwa na wanajeshi kikosi cha 516 kambi ya Kizumbi.

                                     










CHANZO CHA KUKITHIRI KWA MAUAJI YA VIKONGWE CHABAINISHWA

MKUU wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya.


  
  KUSHAMIRI  kwa matukio hayo ya mauaji kwa kukatwa mapanga kwa akina mama katika mkoa wa  Shinyanga kwa asilimia kubwa kunasababishwa na viongozi wa serikali za vijiji ambao hukosa uzalendo kutokana na  kugeuza matukio hayo kuwa vyanzo vya mapato yao kwa kuwahifadhi watuhumiwa wa vifo hivyo ambavyo hudaiwa husababishwa na imani za kishirikina..
Mkuu huyo wa wilaya, aliwashutumu viongozi wa  serikali za vijiji kwa kutokuwa waadirifu na kusahau miiko yao ya uongozi kwa kuwakumbatia wauaji wa akina mama ambao wengi huuawa kuanzia miaka 45 huku wakitambua fika tabia hizo zinakwamisha jitihada za serikali za kuwatia mbaroni na kuwafikisha mbele ya sheria wahusika hao.

ULEVI WAMPONZA BABA,MTOTO AANZA KUMCHARANGA KWA MAPANGA KWA KUCHOSHWA NA UNYWAJI WAKE

MKAZI wa kijiji cha Ndala, Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya, Andondile Mwasamlagila (50) amenusulika kufa baada ya kucharangwa na mapanga na mtoto wake, Yuda Mwasamlagila kutokana na ulevi wa kupindukia.
Wakizungumza na blog hii, wanafamilia walisema kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 11 mwaka huu majira ya jioni ambapo mzee huyo akiwa amejituliza katika makazi yake, akivamiwa na kushambuliwa na mapanga na mtoto huyo.
Walidai kuwa walisikia kelele za kuomba msaada kutoka kwa mzazi huyo wakati akishambuliwa na kwamba waliposogea karibu walikuta akiwa hajitambui huku akiwa na majeraha kwenye shingo na sehemu za kichwa.
Kwa mujibu wa wanafamilia hao, walimkimbiza katika kitu cha afya cha Mwakaleli kwa ajili ya matibabu na kwamba sasa anaendelea vizuri.
Kwamba, wakati majeruhi akipatiwa matibabu, wanakijiji waliamua kwenda kumsaka mtoto wake aliyesababisha tukio hilo ambapo walimkamata akiwa amejificha kwenye shimo huku akiwa amelewa.
Kaimu mganga mfawidhi wa kituo hicho, Dk. Iddy Suleiman alikiri kupokea majeruhi huyo, akisema bado anaendelea na matibabu

HABARI HII NI KWA MSAADA WA eddymoblaze.blogspot.com.

YULE ASKOFU (MBABE WA IMANI) ALIYEBURUZWA MAHAKAMANI NA WAUMINI WAKE SHINYANGA ASHINDWA KESI

Waumini wa kanisa la EAGT Majengo manispaa ya Shinyanga wakimshangilia mchungaji wao David Mabushi baada ya kushinda kesi ndogo kupinga kuvuliwa uongozi wake ndani ya kanisa hilo.Kesi hiyo ilifunguliwa na waumini wa kanisa hilo wakishirikiana na mchungaji huyo dhidi ya kumpinga askofu wa kanda ya magharibi Rafael Machimu ambaye aliwafukuza wachungaji wanane na kulaumiwa na waumini ambapo kesi hiyo iliendeshwa mahakama ya wilaya shinyanga chini ya hakimu Thomson Mtani ikiwa kesi ndogo imekwisha na kesi ya msingi itaanza kusikilizwa tarehe 29/septemba mwaka huu na kesi ndogo imekwisha tolewa maamuzi kuwa mchungaji huyo aendelee na kazi yake kama kawaida. 

Aliyevaa suti ya kijivu ndiyo askofu wa kanda Rafael Machimu aliyefikishwa mahakamani kwa kosa la kufukuza wachungaji kinyume na katiba ya kanisa kwa maslahi yake binafsi,na hapo katika picha akiwa na wapambe wake akitoka mahakamani .

Waumini wa kanisa la EAGT wakiwa wamembeba mchungaji wao David Mabushi baada ya kuruhusiwa na mahakama kuendelea na uchungaji wa kondoo wa mungu mpaka pale kesi yake ya msingi itakaposikilizwa tena,hapo pichani wakiwa nje ya kanisa baada ya kutoka mahakamani. 

Hapo waumini wakimpokea mchungaji wakati akitoka mahakamani na kuelekea kanisani.


wakiendelea kuchangilia kwa kushinda kesi ndogo.


Waumini wa kanisa la EAGT wakitoka nje ya mahakama ya wilaya ya Shinyanga huku wakiwa na nyuso za furaha baada ya mchungaji wao kuruhusiwa kuendelea na shughuli za uchungaji mpaka pale kesi ya msingi itakapo malizika.

Furaha ikiendelea
Umati wa waumini uliokuwa ukisubiria nje ya mahakama .
Huyu Askofu Rafael Machimu akituhumiwa kwa kuchukua maamuzi yake bila kufutata katiba ya EAGT na kuwafukuza wachungaji ambapo ndio alikuwa akienda mahakamani kwa furahama.

waumini wasema ushindi katiba lazima ifuatwe.

Askofu Machimu akiwa na mke wake mwenye nguo za rangi ya njano na bluu pamoja na wapambe wake akiwa nje ya mahakama ya wilaya siku ya jumatatu wakisubiri shauri dogo nje ya mahakama ya wilaya ya Shinyanga mwanzoni mwa wiki hii.-Picha zote na Chibura Makorongo-Shinyanga

MWILI WA MTOTO ALIYEBAKWA NA KUUAWA KINYAMA -SHINYANGA WAZIKWA

Mazishi ya mwanafunzi aliyeuawa kikatili kwa kubakwa kisha kutobolewa macho na watu wasiofahamika kisha mwili wake kutupwa kichakani katika kijiji cha Nhelegani kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga yamefanyika katika makaburi ya familia katika kijiji cha Negezi kata ya Mwawaza katika manispaa ya Shinyanga.

Mwanafunzi huyo  aliyekuwa anasoma darasa la tatu katika shule ya Msingi Negezi iliyopo kata ya Mwawaza manispaa ya Shinyanga alikutwa ameuawa kwa kubakwa kisha kutobolewa Agosti 25 mwaka huu saa saba mchana katika kitongoji cha Kashampa kijiji cha Nhelegani kata ya Kizumbi.


Akizungumza wakati wa mazishi ya mwili wa marehemu  yaliyofanyika leo mchana naibu meya wa manispaa ya Shinyanga David Nkulila alilaani kitendo cha kinyama alichofanyiwa mtoto huyo huku akiitaka jamii kushirikiana na jeshi la polisi katika kuwafichua wahusika wa mauaji hayo.

“Kifo cha mtoto huyu ni mapenzi ya mungu yaliyosababishwa na wanadamu wabaya,naomba suala la hili lifuatiliwe hatuhitaji siasa katika hili inauma sana kwani vitendo vya ukatili dhidi ya watoto vinatishia amani Shinyanga”,alieleza Nkulila.

 Kwa upande wake Intelijensia mkoa wa Shinyanga Bundala Maige alisema suala la ulinzi kwa watoto ni jamii nzima na kwamba wahalifu wako ndani ya jamii hivyo kuitaka jamii kuwafichua wahalifu hao ili kukomesha vitendo vya ukatili vinavyoendelea mkoani Shinyanga.


Naye mwenyekiti wa mtaa wa Masekelo kata ya Masekelo yalikofanyika mazishi ya mtoto huyo bwana Peter Juma Kitundu alisema kifo cha mtoto huyo kinatia simanzi kubwa kwani kimesababishwa na binadamu huku akiiomba serikali kulifanyia uchunguzi wa kina tukio hilo  na lisiingizwe suala la siasa.

Kwa upande wake mwinjilisti  Emmanuel Donald Kaswalala aliyeendesha ibada ya mazishi alilaani vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa watotot huku akiiomba jamii kumrudia mwenyezi mungu kwa kuondokana na matendo mabaya.

KUNDI LA PANYA LAMSHAMBULIA MTOTO WA MWEZI MMOJA VIUNGO VYAKE VYA MWILI.

Taarifa kutoka mjini Johannesburg Afrika Kusini zinasema - kuwa panya walimng'ata mtoto wa mwezi mmoja vidole na pua .
Mtoto huyo anasubiri kufanyia upasuaji wa kuumba maumbile yake ya usoni baada ya tukio hilo huko Alexandra, Johannesburg .

KIKONGWE AUWAWA KWA IMANI ZA KISHIRIKINA, ACHARAZWA MAPANGA.


Kikongwe mwenye umri wa miaka 62 Raheli Jilungu mkazi wa kijiji cha Mishepu katika halmashauri ya wilaya ya  Shinyanga aliuawa kwa kukatwa shingo na mtuhumiwa aliyetambulika kwa jina la Maganga Fuja akiwa na wenzake
watatu .Chanzo cha mauaji hayo ni imani potofu za  kishirikina. 

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga  Justus Kamugisha atoa wito kwa wakazi wa mkoa wa Shinyanga kupambana na vitendo vya mauaji ya vikongwe.Kamugisha alisema kazi kubwa hivi sasa kwa upande wake kuhakikisha mauaji yanakoma mkoani Shinyanga.alisema ufanisi wa mapambano hayo  yanategemea  ushirikiano kutoka kwa wakazi wa mkoa wake kwa kutoa taarifa za wausika wa mauaji hayo.alisema mauaji hayo yamekuwa na mtandao mkubwa wakiwemo ndugu wa marehemu wanaofanyiwa vitendo hivyo. 
Pia  kuanzia Januari mpaka desemba  mwaka 2013  mkoa ulikuwa na mauaji ya vikongwe 27 huku watuhumiwa 16 wakifikishwa mahakamani na kuanzia mwezi Januari hadi  Julai mwaka huu vikongwe 11 wameuwawa huku watuhumiwa 16 pia wakifikishwa mahakamani.

RACHAL MASHISHANGA AUKWAA UENYEKITI BAWACHA MKOA WA SHINYANGA CHADEMA

HUYU HAPA NI RACHAL MASHISHANGA  MBUNGE VITI MAALUMU CHADEMA MKOANI SHINYANGA AMEUKWAA UENYEKITI WA BAWACHA  CHADEMA MKOA.CHAMA  Cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA),mkoani Shinyanga hatimaye kimepata viongozi wapya wa mkoa ,ikiwa imepita miaka mitatu bila ya kuwa na mwenyekiti wa mkoa wa Chama hicho ikiwa  wamemchagua  Peter Frank kuwa mwenyekiti kushika nafasi ya aliyekuwa  mwenyekiti  phlipo Shelembi aliyefariki  dunia mwaka 2011.

MWANAFUNZI WA DARASA LA TATU,ABAKWA,ATOBOLEWA MACHO NA KUUWAWA.

MWANAFUNZI wa darasa la tatu  katika shule ya msingi Negezi iliyopo kata ya Ndala aliyefahamika kwa jina la Happy Kashidye (9), Mkazi wa Kata hiyo Manispaa ya Shinyanga siku ya jumapili  tarehe 24 ,aliuawa na watu wasio julikana  kisha  kumfanyia kitendo cha kumbaka na  kumtoboa Macho.
Licha ya kata hiyo, pia wimbi la kuwabaka watoto na kuwatoboa macho linaonekana kuendelea manispaa ya Shinyanga ikiwa baadhi ya wananchi  kama wanaovyooneka kwenye picha kuonesha kukerwa na kitendo hicho  huku wakiitaka serikali kuliangalia suala hilo kwa ulinzi mkubwa .

WAUMINI WA KANISA LA EAGT WAANDAMANA KUMKATAA ASKOFU WA KANISA HILO.

ASKOFU  wa kanisa  la EAGT kanda ya magharibi Rafael  Machimu  amefikishwa mahakamani  na waumini wa kanisa hilo kwa kitendo cha  kumpinga  kumfukuza  mchungaji wao  David Mabushi  bila kutenda kosa lolote jambo ambalo walilieleza ni  kwenda  kinyume na taratibu.

Waumini hao wakizungumza kwa nyakati tofauti na waandishi wa habari walisema wameamua kumfikisha mahakamani Askofu huyo wakipinga kitendo cha  mchungaji wao na kudai kuwa hakuna kipengele kilichoainishwa cha kumwondoa mchungaji bila kosa.

WATOTO WENYE ULEMAVU WA NGOZI WAONGEZEKA KWA KASI KITUO CHA BUHANGIJA KWA HOFU.

Meya  wa manispaa ya Shinyanga  Gullamu Hafidh Mkadamu akiwa meza kuu na   msimamizi ambaye ni mwalimu Peter Ajali wa shule hiyo akikabishiwa fimbo nyeupe 11 za watoto wasioona huku akielezwa wimbi la kuongezeka kwa watoto wenye ulemavu wa ngozi kila siku watoto watatu mpaka wanne.
MKAMA SHAKENGWA  NI KIONGOZI KATIKA KITUO CHA KULELEA WATOTO WENYE  ULEMAVU MBALIMBALI CHA BUHANGIJA   WAKIWEMO ALBINO.  WATOTO wenye ulemavu  wa ngozi  katika kituo maalumu cha kulea  watoto hao Buhangija manispaa ya Shinyanga ,wamezidi kuongezeka kituoni hapo  kutokana na wimbi la mauaji y a albino  kuibuka tena na kufikia watoto zaidi ya  100  kupelekwa hapo kutoka maeneo mbalimbali kwa hofu ya kuuwawa na kufanyiwa  ukatili.

SHIDA YA MAJI WATOTO WASHINDISHWA KWENYE VISIMA,WAZAZI WASAKA MAJI NYAKATI ZA USIKU.

WAKAZI wa kitongoji cha Mwabagikulu katika Kjiji cha  Ikonongo kata ya Salawe halmashauri ya wilaya ya Shinyanga  wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji hali ambayo inawafanya wakazi wa kijiji hicho  kuamka   nyakati za usiku kutafuta maji huku wakiwa na hofu ya kuhatarisha maisha yao,ambapo mkazi mmoja wa kijiji hicho Ndelemo Maguta alisema kuwa inawalazimu kutafuta maji nyakati za usiku  sababu ukienda majira ya mchana hakuna maji  huku watu ni wengi,wengine utakuta wanawatuma watoto kwenda kushinda  kwenye visima vya maji  wakisha jaza huwafuata.
Watoto hawa sio kwamba wanacheza bali kutokana na shida ya maji kwenye  kitongoji cha mwabagikulu kijiji  cha Ikonongo  kata ya Salawe halmashauri ya wilaya ya Shinyanga  wamekuwa wakitumwa na wazazi wao na kushinda kwenye visima kwaajili ya  kutafuta maji .

WATUHUMIWA SABA WA MAUAJI YA ALBINO WAKAWAMATWA BARIADI AKIWEMO MGANGA WA KIENYEJI.

Mkuu wa wilaya ya Bariadi  Erato Sima ambaye ni mwenyekiti wa ulinzi na usalama wilayani humo.

JESHI la polisi mkoani Simiyu limefanikiwa kuwakamata watu saba wanaodhaniwa  kuwa wauwaji wa aliyekuwa mlemavu  wa ngozi (albino) Munghu Mugata (40) aliyeuwawa kwa kukatwa mapanga  mnamo mwezi mei huko katika  kijiji cha Gasuma kata mwaubingi wilayani  bariadi.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Kudawa Yelema (52) ambaye ni mganga wa jadi, Sitta Maduhu (39), Jasamila Sungwa (42), Mpamba Saguda (18), Dede Madono (54), Majeshi Sunja (38), pamoja na Mabula Bindondo (52) wote wakulima na wakazi wa kijiji cha Gasuma

Akiongea na waandishi wa habari ofisi kwake, mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa ambaye pia ni mkuu wa mkoa Paschal Mabiti, alisema kuwa kati ya watuhumiwa hao mmoja ni mganga wa jadi.

MAKAMPUNI YA UNUNUZI WA ZAO LA PAMBA YAONJA JOTO YA JIWE SOKO LA DUNIA.

BAADHI ya makampuni ya ununuzi wa zao la pamba mkoani Shinyanga  yameonesha kujitoa kuendelea na ununuzi huo kwa kudai kuwa soko la dunia limeshuka  hawatapata faida ambapo chama kikuu cha ushirika  mkoani humo( Shirecu) kimeendelea na ununuzi  huo na kufikia kilo millioni 4.8 ikiwa lengo lake kwa mwaka huu ni kufikia kilo zaidi ya  millioni 8.
Mojawapo ya kampuni lililojitoa na ununuzi huo ni kampuni ya Ahamu kwa kuona itapata hasara ambapo  asilimia 75 ya wakulima wamejitokeza kuuza pamba yao huku asilimia 25 wakisubiri huenda soko litakuwa zuri ikiwa bei iliyopo hivi sasa ni shilingi 750 kwa kilo moja.

CHANGAMOTO YA KUKOSA SOKO LA UHAKIKA KWA WAKULIMA CHANZO CHA UMASIKINI.

WAKULIMA WAKIWA SHMABANI WAKIVUNA ZAO LA DENGU KATIKA KIJIJI  CHA AMANI KATA YA SALAWE HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA.

WAKIBEBA ZAO LA DENGU NA KUPELEKA NYUMBANI KWA KUCHAMBUA.
WAKULIMA  wa zao la dengu katika kijiji cha  Amani kata ya Salawe halmashauri ya wilaya ya  Shinyanga  bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa  soko la uhakika  kwenye  zao hilo ikiwemo miundombinu ya barabara kuwa mibovu hali ambayo inawafanya kushindwa kusafirisha mazao yao.

Wakiongea na mwandishi wa habari aliyetembelea wakulima wa kijiji hicho walisema  kuwa zao hilo limekuwa mkombozi katika kunyanyua pato la familia  lakini kubadilika kwa  bei  ikiwa  wengine wanauza shilingi 45,000 mpaka 55,000 kwa gunia moja na kukosa soko la uhakika  imekuwa ni tatizo,  ikiwemo wadudu wahalibifu pamoja na panya.

WIZI WA NYAYA ZA SIMU WASABABISHA HASARA YA ZAIDI YA SHILINGI MILLIONI 133 MANISPAA YA SHINYANGA.

BAADHI ya wananchi manispaa ya Shinyanga  wametakiwa kuwapatia elimu zaidi  vijana  na kuondoakana na uhalifu ambao chanzo chake ni utumiaji wa  madawa ya kulevya, biashara ya vyuma chakavu ikiwemo wizi wa  nyaya za simu hali ambayo imefanya shirika la mawasiliano  ya umma nchini TTCL kwa wilaya  shinyanga kupata hasara ya zaidi ya shilingi million 133.

MBWA AMTAFUNA MWANAFUNZI WA DARASA LA TATU NA KUPOTEZA MAISHA

Moja ya mbwa anayedaiwa kumla mtoto Ibrahim Faraja Chipungahelo (9) akiwa ameuawa pia.

MWANAFUNZI wa Shule ya Msingi Ludewa mkoani Njombe, Ibrahim Faraja Chipungahelo (9) ameuawa kikatili na mbwa wanaosadikiwa kuwa na kichaa kisha kuliwa nyama. 


Tukio hilo lililoacha simanzi kubwa kwa wakazi wa Ludewa mjini lilijiri saa 7 mchana wa Agosti 8, mwaka huu katika eneo la Ikilu ambapo marehemu na wenzake walikuwa wakipita nje ya nyumba ya mtu aliyejulikana kwa jina la Bosco Lingalangala (Boli) kwenda kuchuma mapera sehemu.
o.
DAKTARI ALIVYOSEMA
Kwa mujibu wa taarifa ya Dokta Sira Rajabu wa Hospitali ya Wilaya ya Ludewa aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu Ibrahim, ulikuwa na majeraha makubwa mwili mzima huku paja la mguu wa kulia likiwa limeondolewa nyama kabisa.
MGANGA WA MIFUGO
Akizungumza na paparazi wakati wa msiba wa mtoto huyo, Mganga wa Mifugo wa Wilaya ya Ludewa, Simon Haule alisema mbwa hao walikuwa hawajapata chanjo kwa zaidi ya miaka miwili. Kwa hiyo tayari walikuwa na ugonjwa wa kichaa ambacho kisingeweza kupona tena zaidi ya kuwaua.

Padri akiiombea roho ya mtoto, Ibrahim Faraja Chipungahelo ikapate kupumzika kwa amani.

WANANCHI WAANDAMANA, WAWAUA MBWA
Kufuatia tukio hilo la kusikitisha, Agosti 10, mwaka huu baadhi ya wananchi wa Kata ya Ludewa waliandamana ili kushinikiza haki itendeke baada ya kuambiwa kuwa mmiliki wa mbwa hao alitishia kumshtaki yeyote ambaye angehusika kuwaua mbwa wake.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano wa dharura ulioitishwa na Diwani Mchilo, wananchi hao walisema mbwa hao walikuwa tishio kwa muda mrefu kwani walishateketeza mifugo mingi wakiwemo mbuzi 22 na ndama 1, lakini cha kushangaza kila walipolipeleka suala hilo kwenye vyombo vya dola, mmiliki alitaka ushahidi.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wananchi hao walisitisha mkutano huo na kuandamana mpaka kwenye nyumba ya mmiliki wa mbwa hao ambapo waliwaua kwa kuwapiga risasi.
MIZOGA MITAANI
Kwa hasira, waliondoka na mizoga na kupita nayo mitaani huku wakiimba nyimbo mbalimbali za kikabila na kawaida.
WACHOMA MOTO MIZOGA
Baada ya kuzunguka na mizoga ya mbwa hao kwa muda mrefu, mwishowe walikwenda kwenye ofisi ya kata ambako waliichoma moto na kuiteketeza kabisa huku wakishangilia.
MKUU WA WILAYA
Kufuatia tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Ludewa, Juma Madaha ameviagiza vyombo husika ikiwemo idara ya kilimo na mifugo na jeshi la polisi kuchukuwa hatua za kisheria kwa yeyote anayehusika na tukio hili akiwemo mmiliki wa mbwa hao.
Marehemu Ibrahim Faraja Chipungahelo alizikwa Agosti 9, mwaka huu kwenye Makaburi ya Ludewa, Njombe.

Wananchi wakichoma mwili wa mbwa aliyemuua mtoto Ibrahim.
KAMANDA WA POLISI
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, ACP Fulgensi Ngonyani alikiri kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa upelelezi unaendelea sanjari na kuwahoji watu mbalimbali, akiwemo mmiliki wa mbwa hao anayeishi jijini Dar es Salaam.Mungu ailaze pema peponi, roho yake. Amina.
KARENY. Powered by Blogger.