Habari za hivi Punde

UHABA WA MAJI KWENYE KITUO CHA AFYA CHA IKONONGO WAWATESA MAMAWANAOKWENDA KUJIFUNGUA KITUONI HAPO.

Mgonjwa aliyelazwa katika kituo cha afya cha Ikonongo kata ya Salawe akumbana na  changamoto ya ukosefu wa maji kituoni hapo.


Hiki ni kituo cha afya cha kilichopo kijiji cha  Ikonongo  kata ya Salawe kinachokabiliwa na  uhaba mkubwa wa maji.

KITUO cha afya kilichopo kijiji cha  Ikonongo kata ya Salawe halmashauri ya wilaya  ya Shinyanga  kinakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji hali ambayo inawafanya mama wanaotaka kujifungua  kwenda na maji ikiwemo ndugu wanaowasindikiza kuhaha kutafuta maji  umbali wa kilomita mbili ili waweze kufulia nguo  baada ya kuwa wamejifungua  hospitalini hapo.
Wakiongea na mwandishi wa habari aliyetembelea kwenye kituo hicho baadhi ya mama waliojifungua  na wagonjwa walisema kuwa wanalazimika kwenda na maji kutokana na shida ya upatikanaji wa maji katika kituo hicho  hata ya  kumezea dawa hakuna mpaka wakanunua ikiwa wengine hawanapesa.


Naye mwenyekiti wa kijiji cha Ikonongo  Twiga Mashimba alisema kuwa uhaba wa maji upo  wagonjwa wanateseka hata ya kumezea dawa shida,mama wanaokuja kujifungua hulazimika kwenda na maji wakati mwingine walikuwa wakichota kwenye malambo nayo yamekauka hivyo hulazimika ndugu kufuata umbali wa kilomita mita mbili.
“Licha  ya kufuata huko  maji wengine huvizia nyakati za usiku  kwa kujikokoteza kwenye chemchem yanayotoka polepole  ili kupata maji karibu , jambo ambalo linahatarisha maisha yao kwa usalama ,ikiwa tatizo hili limekuwa la muda mrefu hivyo tunaiomba serikali kutatua kero hii na kuweza kunusuru afya za wagonjwa ikiwemo mlipuko wa magonjwa kama kipindupindu kwa maji yanayopatikana   ni machafu  sio salama”alisema mwenyekiti wa kijiji.
Naye muuguzi katika kituo hicho Yusuph Adonji alisema kuwa  uhaba wa maji upo mama wanaokuja kujifungua hulazimika kuja na maji au ndugu  zao kufuata umbali wa kilomita mbili,maji yanayopatikana kituoni hapo siyo kwaajili ya wagonjwa au mama wanaojifungua bali ni kwa watumishi  kwaajili ya kujisafisha na kufanyia usafi kwa upigaji deki.
Mganga  mkuu katika kituo hicho   dkt Saimon Wilson  alikiri kuwepo kwa changamoto ya uhaba wa maji kituoni hapo huku akieleza kuwa   wamekuwa wakitumia gari kuleta maji  wakati mwingine kumpatia mtu kiasi cha shilingi 5000 na kujaza mapipa yaliyopo kwani awali kulikuwepo  tanki na mashine ya kusukumia maji, lakini tanki lilihamishwa  baada ya  mashine kuharibika.
Kituo hiki kwa siku kinahudumia wagonjwa  kati ya 40 hadi 50,kwa mwezi  ni watu zaidi ya 25,000 wakiwemo mamawanaojifungua  kutoka vijiji vya Amani,Songambele,Ikonongo Zonza na Zunzuli ambapo maeneo hayo yote hayana zahanati na changamoto iliyopo uhaba wa maji hutumia  gari  la wagonjwa kama likiishiwa mafuta hutumia watu kusomba maji na kuwalipa pesa.

0 Response to " UHABA WA MAJI KWENYE KITUO CHA AFYA CHA IKONONGO WAWATESA MAMAWANAOKWENDA KUJIFUNGUA KITUONI HAPO."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.