Habari za hivi Punde

CHANGAMOTO YA KUKOSA SOKO LA UHAKIKA KWA WAKULIMA CHANZO CHA UMASIKINI.

WAKULIMA WAKIWA SHMABANI WAKIVUNA ZAO LA DENGU KATIKA KIJIJI  CHA AMANI KATA YA SALAWE HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA.

WAKIBEBA ZAO LA DENGU NA KUPELEKA NYUMBANI KWA KUCHAMBUA.
WAKULIMA  wa zao la dengu katika kijiji cha  Amani kata ya Salawe halmashauri ya wilaya ya  Shinyanga  bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa  soko la uhakika  kwenye  zao hilo ikiwemo miundombinu ya barabara kuwa mibovu hali ambayo inawafanya kushindwa kusafirisha mazao yao.

Wakiongea na mwandishi wa habari aliyetembelea wakulima wa kijiji hicho walisema  kuwa zao hilo limekuwa mkombozi katika kunyanyua pato la familia  lakini kubadilika kwa  bei  ikiwa  wengine wanauza shilingi 45,000 mpaka 55,000 kwa gunia moja na kukosa soko la uhakika  imekuwa ni tatizo,  ikiwemo wadudu wahalibifu pamoja na panya.


Wakulima  kutoka kijiji cha Amani  Josephati Mahona  na Mariamu Kihembe walisema   kuwa changamoto imekuwepo, wakati wa kukomaa  kwa  zao hilo likiwa  shambani kwa kuliwa na wadudu ambapo hutumia gharama ya kiasi  cha shiling  6000  kununulia dawa za kuua wadudu.

“Kwa kweli zao hili ni mkombozi kwenye familia hakuna zao lingine tunalolitegemea linalokomaa kwa muda mfupi na kuuza,lakini kumekuwepo na changamoto  ya soko kukosa uhakika, wakulima tumekuwa tukijitafutia  soko kama kuku wa kienyeji serikali imetusahau,pia hata hawa walanguzi wamekuwa wakitudhulumu kwa kiasi kikubwa ikiwa nasi tumetumia gharama kubwa katika maandalizi”alisema Mahona.

Naye Twiga Mashimba  mkulima wa zao hilo  alisema  kuwa  zao  la dengu linaanza kulimwa mwezi march na mavuno yake ni kipindi cha kuanzia mwezi wa saba hivyo changamoto  za usafirishaji na soko kubadilikabadilika kumekuwa kukimnyima fursa mkulima  kufahamu bei halisi kwani walanguzi wao huenda kuuza kwa gharama ya shilingi 70,000 kwa gunia moja.

Mwenyekiti wa kijiji cha Amani  Dotto Polepole  alisema   kuwa  licha ya wakulima kulilima zao hilo na kutegemea kuongeza kipato ndani ya familia kumekuwa na changamoto ya  kuwepo kwa miundombinu mibovu kwenye usafirishaji wa mazao ambapo wakulima wengi wamekuwa wakipeleka jijini Mwanza  na kuona ndio karibu na unafuu kwao kuliko shinyanga mjini.

Ofisa kilimo wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga  Oscar Jeremiah alisema  kuwa  zao hilo linaathiriwa na unyevunyevu  liwapo ardhini  na hufanya kuoza ikiwemo wadudu wahalibifu kama funza na panya  hiyo imekuwa ni changamoto.

Ofisa kilimo huyo alisema  kuwa kilimo cha zao la dengu  kinaanza mwezi March kipindi mvua zimeanza kupungua  kwani linahitaji mvua za wastani,  kwa mwaka huu matarajio yalikuwa ni kulima hekta 8,644 na mavuno tani 5,108 lakini imefikia katika uhalisia  eneo lililolimwa kwa mwaka huu ni hekta 3,881 na mavuno halisi ni tani 2,293.






0 Response to "CHANGAMOTO YA KUKOSA SOKO LA UHAKIKA KWA WAKULIMA CHANZO CHA UMASIKINI."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.