Habari za hivi Punde

WIZI WA NYAYA ZA SIMU WASABABISHA HASARA YA ZAIDI YA SHILINGI MILLIONI 133 MANISPAA YA SHINYANGA.

BAADHI ya wananchi manispaa ya Shinyanga  wametakiwa kuwapatia elimu zaidi  vijana  na kuondoakana na uhalifu ambao chanzo chake ni utumiaji wa  madawa ya kulevya, biashara ya vyuma chakavu ikiwemo wizi wa  nyaya za simu hali ambayo imefanya shirika la mawasiliano  ya umma nchini TTCL kwa wilaya  shinyanga kupata hasara ya zaidi ya shilingi million 133.

Suala la unyang’anyi na wizi kwa vijana kwenye maeneo ya makazi limekithiri  hasa kwenye upande wa  wizi za nyaya  za simu ambao umekosa ulinzi, watu kudiriki kufanya vitendo vya kufua nyaya karibu na makazi  hivyo  shirika la TTCL  katika eneo  la kata ya  ndembezi,Ngokolo  zilizibiwa cable urefu wa mita 200 na kupatikana  hasara ya zaidi  shilingi millioni sita.

Hayo yalisemwa  na  naibu meya  wa manispaa hiyo David Nkulila ambaye pia ni diwani wa kata ya Ndembezi  pamoja na  ofisa ufundi kutoka shirika hilo  Madunda  Madunda  kwenye mkutano wa hadhara uliohusisha  kata tatu za mjini,Ngokolo na Ndembezi  na kufanyika katika shule ya msingi Bugoyi A iliyopo eneo la mtaa wa Mbuyuni  kata ya Ndembezi.

Nkulila alisema kuwa uhalifu umezidi kuongezeka sababu ya vijana  wengi kujiingiza kwenye  utumiaji wa madawa ya kulevya  na biashara ya vyuma chakavu ambao umeipatia hasara TTCL, aliwata wananchi kuchukua hatua za haraka kuwaonya vijana wao ikiwemo biashara  hiyo  ambayo imekuwa ni chanzo kikubwa cha uhalifu kwenye maeneo mengi.

“Mimi nasema kuwa madawa ya  kulevya vijana wengi wamekuwa wakiyatumia  kwa kisingizo cha kukosa ajira, hilo sio kweli bali  wanayatumia ikiwa wazazi na walezi wakishuhudia  na mwisho wake  kufanya uhalifu,pia vilabu vya  pombe za kienyeji  na baa  kutokufungwa  bila kuzingatia muda nao unachangia hivyo atakaye kiuka  utaratibu huu achukuliwe hatua za kisheria”alisema  Nkulila.

Naye  Madunda katika mkutano huo  alisema kuwa nyanya nyingi zimeibiwa ni zile za kuunganishiwa wateja  ambapo alidai kuwa suala la wizi lilikithiri  hali ambayo inaonekana shirika la TTCL  linataka kuhujumiwa kwa njia hiyo, kwani wizi unatendeka  maeneo yaliyo karibu na makazi bila kutoa ushirikiano wa wananchi kwenye eneo husika isitoshe jeshi la polisi nao wakiwepo.

0 Response to "WIZI WA NYAYA ZA SIMU WASABABISHA HASARA YA ZAIDI YA SHILINGI MILLIONI 133 MANISPAA YA SHINYANGA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.