Habari za hivi Punde

MAKAMPUNI YA UNUNUZI WA ZAO LA PAMBA YAONJA JOTO YA JIWE SOKO LA DUNIA.

BAADHI ya makampuni ya ununuzi wa zao la pamba mkoani Shinyanga  yameonesha kujitoa kuendelea na ununuzi huo kwa kudai kuwa soko la dunia limeshuka  hawatapata faida ambapo chama kikuu cha ushirika  mkoani humo( Shirecu) kimeendelea na ununuzi  huo na kufikia kilo millioni 4.8 ikiwa lengo lake kwa mwaka huu ni kufikia kilo zaidi ya  millioni 8.
Mojawapo ya kampuni lililojitoa na ununuzi huo ni kampuni ya Ahamu kwa kuona itapata hasara ambapo  asilimia 75 ya wakulima wamejitokeza kuuza pamba yao huku asilimia 25 wakisubiri huenda soko litakuwa zuri ikiwa bei iliyopo hivi sasa ni shilingi 750 kwa kilo moja.

Wakiongea na mwandishi wa habari kwa nyakati tofauti  mjini Shinyanga meneja wa  shirecu Joseph Mihangwa alisema kuwa  kweli wanunuzi wengi wamejitoa  ila kupitia chama chake wanaendelea  kununua na kufikia  kilo millioni 4.8 na malengo  ni kilo millioni 8,huku mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Ngassa Mboje  alisema wakulima  wadogowadogo wamejitokeza kuuza lengo kupata fedha na kukithi mahitaji ndani ya familia.
‘Shirecu  kwa malengo hayo inatarajia kuyafikia ikiwa makampuni mengine yamejitoa sifahamu sababu ni kitu gani  kujitoa kwao,lakini soko la dunia  limekuwa baya  kwa kuangalia bei iliyopo  hata hii ya shilingi 750  tunayonunua  kutoka kwa mkulima  ni kubwa hivyo tunanunua kwa matumaini huenda  soko la dunia bei yake ikawa nzuri”alisema.
Mihangwa alisema kuwa changamoto ya mizani  kwa upande wao hakuna tatizo kwani imekuwa ikisimamiwa na vyama vya msingi vya ushirika  kwa usahihi ikiwa kuna vyama 480 vilivyochini ya shirecu ambapo kati ya hivyo  210 vilivyojiimarisha  kwenye biashara huku vilivyobaki vimeteteleka kutokana  uchumi wake  kutokuwa mzuri.
Naye  Ngassa  Mboje  alisema kuwa  baadhi ya wakulima wakubwa wa zao la pamba  hawajajitokeza kuuza wakisubiri soko kuwa zuri huku msimu ukienda mwishoni,  lakini wakulima wadogo waliowengi wamejitokeza  kuuza kwa bei ya shilingi 750 lengo waweze kupata fedha za kujikimu ndani ya familia zao.
Hata hivyo Diwani wa kata ya Mondo  wilayani Kishapu mkoani  Shinyanga  John Ndama  alisema kuwa  wakulima wamekosa ujanja  imebidi wauze kwa bei hiyo ikiwa kampuni  inayojulikana  Villani ilianza kununua pamba kwenye baadhi ya maeneo kwa shilingi  800 kwa kilo moja  ambapo kampuni ya  jambo ilijitoa na baadaye kurudi na kampuni ya  Ahamu  imekwisha jitoa jumla kwenye ununuzi huo.
Nao wakulima  wa  zao la pamba  mkoani Shinyanga  akiwemo  Maduhu Shija na Bernadetha  Joshua walisema kuwa  wakulima wamekubali kununua kwa bei  ya shilingi 750 kwa kilo kutokana na changamoto kubwa  ndani ya familia ,hata kujitoa kwa  baadhi ya makampuni  kununua zao hilo wako sahihi kwani wameona  wanapata  hasara pia.


0 Response to "MAKAMPUNI YA UNUNUZI WA ZAO LA PAMBA YAONJA JOTO YA JIWE SOKO LA DUNIA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.