Habari za hivi Punde

KAMATI YA MAJI YAFIKISHWA MAHAKAMANI KIJIJI CHA SONGAMBELE KATA YA SALAWE KWA UBADHIRIFU.

BAADHI  ya wananchi wa kijiji cha Songambele kata  ya Salawe halmashauri ya wilaya ya Shinyanga   wamedai kutosomewa mapato na matumizi  ya mradi wa maji  ziwa victoria na kufanya upotevu  wa kiasi cha zaidi ya shilingi millioni  nane hali  ambayo imefanya mtendaji wa kijiji  Paschal Chuma  Kusimamishwa kazi  na kamati  ya usimamizi wa maji kufikishwa mahakamani.
Hata hivyo  inadaiwa kuwa kwa mwezi walikuwa wakikusanya kiasi cha shilingi millioni 1.6 katika kituo kikubwa  na kituo kidogo ni kiasi cha shilingi millioni 1.5, lakini katika akaunti ya benki kulikuwa  na kiasi cha shilingi laki tatu  ikiwa mradi huo  ulizinduliwa mwezi wa tano mwaka 2008.
Wakiongea na mwandishi wa habari aliyetembelea kijijini hapo,ambapo baadhi ya wananchi akiwemo mwenyekiti wa tawi Songambele  wa chama cha mapinduzi (CCM) Madukwa Gulaka alisema kuwa  changamoto ipo ya kutoitishwa mikutano ya hadhara na kusomewa mapato na matumizi   ya kiasi cha fedha zilizokusanya  ikiwa mradi wa maji umeanza siku nyingi.
Gulakwa alisema kuwa  mara baada ya kusimamishwa  na mkurugenzi wa halmashauri Mohamed Kiyungi  jukumu la usimamizi  na ukusanyaji wa fedha lilipewa sungusungu   na kwa muda wa siku  27 walifanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi millioni 1.3 ikiwa ndoo moja  wanawauzia wananchi kwa shilingi 25.
Mmoja wa wananchi hao Hermani Sanane alisema  tangu kuanzishwe kwa mradi huo hawajawahi kusomewa mapato na matumizi  ya kuhusiana na fedha zinazokusanywa ikiwa ni haki yao kisheria  kuzifahamu lakini kumekuwepo na ubabaishaji mpaka uongozi kutoka halmashauri uliopata malalamiko hayo na kuyachunguza ikaamua  kuwafikisha mahakamati  kamati nzima iliyokuwa na watu wanne.
“Mimi huwa nikisema wananiita muongo mnafiki hakuna mkutano wa hadhara ulioitishwa  na kutusomea mapato na matumizi,mwenyekiti na  mtendaji wa kijiji hujichukulia maamuzi  wenyewe mpaka kufikia  hasara  ya shilingi millioni  nane , na hapo itakuwa ni zaidi maana  mradi huo wa ziwa Victoria  ulizinduliwa mwaka  2008 na kuundwa kwa kamati ya usimamizi na wananchi”alisema  Sanane.
Naye mwenyekiti wa kijiji cha Songambele  Seke Kakonge alisema kuwa  sakata la ukusanyaji wa fedha  za maji kweli mtendaji wa kijiji huyo alisimamishwa na mkurugenzi wakiwemo watu wanne kwenye kamati ya maji  ambao wamefikishwa mahakamani baada ya wakaguzi kukagua na kubaini upotevu wa kiasi cha shilingi million nane.
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri hiyo Ngassa Mboje alisema kuwa  oparesheni ya  kuzikagua  kamati za maji zimeanza na sio kijiji hicho tu bali kwenye maeneo mengi yalipo na kamati za usimamizi wa maji  kwani kumekuwepo na ubadhirifu mkubwa kupitia kamati hizo ikiwa zinachaguliwa na wananchi wenyewe,huku mbunge wa jimbo la Solwa Ahamed Salum akisisitiza  wananchi kusomewa mapato na matumizi kwa muda muafa  na kuchagua  watu  wa kamati  wenye uadilifu.
Mkurugenzi wa halmashauri hiyo  Kiyungi alisema kuwa kweli amemsimamsiha mtendaji wa kijiji hicho kwa kutosimamia vizuri majukumu yake huku  kamati ya watu wanne  wa usimamizi wa maji wakifikishwa mahakamani kwa  kutuhumiwa kufanya upotevu wa fedha,hivyo kilichobainika hapo ni viongozi kutowasomea wananchi mapato na matumizi ndio maana kumekuwepo na kelele nyingi.

0 Response to "KAMATI YA MAJI YAFIKISHWA MAHAKAMANI KIJIJI CHA SONGAMBELE KATA YA SALAWE KWA UBADHIRIFU."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.