Habari za hivi Punde

WIZARA YA AFYA IMEWEKA MIKAKATI YA KUTHIBITI UGONJWA WA EBOLA


WAZIRI wa afya na ustawi wa  jamii   dkt seif Rashidi amesema kuwa jumla ya shilingi Billioni 1.8 kwaajili ya kuthibiti ugonjwa wa ebola ambapo wizara  sambamba na hilo imeweka  mkakati unaoendelea wa kuwabaini watu wenye maambukizi ya virus vya ugonjwa huo katika mipaka ya nchi pamoja na viwanja vya ndege nchini.

Akiongea  Jijini Dar es Salaam, Waziri wa wizara hiyo Dkt. Seif Rashid amesema wizara hiyo imeongeza kiwango cha ufuatiliaji katika maeneo hayo kwa kuwakagua abiria katika viwanja vya ndege vya kimataifa hapa nchini ambapo pia wizara imeagiza kifaa cha Thermoscaner kitakachosaidia kuwabaini wagonjwa wenye dalili za ugonjwa huo.


Dkt. Rashid amesema vifaa vya kujikinga na ugonjwa huo vipo vya kutosha kwa ajili ya matumizi kwa watoa huduma na tayari vimeanza kusambazwa kutoka Bohari ya Dawa MSD kwenda hospitali za wilaya, mikoa na rufaa nchini.

Katika hatua nyingine, Daktari bingwa wa upasuaji wa magonjwa ya ndani katika hospital ya rufaa ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam nchini Tanzania Dkt. Kariameli Wandi ameitahadharisha jamii dhidi ya ugonjwa wa homa ya ini ambao imeonekana kushika kasi hapa nchini huku wananchi wakishindwa kutambua dalili za ugonjwa huo mapema.

Akizungumza na Kurasa leo jijini Dar es Salaam Dkt. Wandi amesema hata matibabu ya ugonjwa wa homa ya ini yamekuwa ni changamoto kutokana na mgonjwa wa homa ya ini kulazimika kutumia dawa za kufubaza ugonjwa UKIMWI, ARVs.


0 Response to "WIZARA YA AFYA IMEWEKA MIKAKATI YA KUTHIBITI UGONJWA WA EBOLA "

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.