Habari za hivi Punde

ULEVI WAMPONZA BABA,MTOTO AANZA KUMCHARANGA KWA MAPANGA KWA KUCHOSHWA NA UNYWAJI WAKE

MKAZI wa kijiji cha Ndala, Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya, Andondile Mwasamlagila (50) amenusulika kufa baada ya kucharangwa na mapanga na mtoto wake, Yuda Mwasamlagila kutokana na ulevi wa kupindukia.
Wakizungumza na blog hii, wanafamilia walisema kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 11 mwaka huu majira ya jioni ambapo mzee huyo akiwa amejituliza katika makazi yake, akivamiwa na kushambuliwa na mapanga na mtoto huyo.
Walidai kuwa walisikia kelele za kuomba msaada kutoka kwa mzazi huyo wakati akishambuliwa na kwamba waliposogea karibu walikuta akiwa hajitambui huku akiwa na majeraha kwenye shingo na sehemu za kichwa.
Kwa mujibu wa wanafamilia hao, walimkimbiza katika kitu cha afya cha Mwakaleli kwa ajili ya matibabu na kwamba sasa anaendelea vizuri.
Kwamba, wakati majeruhi akipatiwa matibabu, wanakijiji waliamua kwenda kumsaka mtoto wake aliyesababisha tukio hilo ambapo walimkamata akiwa amejificha kwenye shimo huku akiwa amelewa.
Kaimu mganga mfawidhi wa kituo hicho, Dk. Iddy Suleiman alikiri kupokea majeruhi huyo, akisema bado anaendelea na matibabu

HABARI HII NI KWA MSAADA WA eddymoblaze.blogspot.com.

0 Response to "ULEVI WAMPONZA BABA,MTOTO AANZA KUMCHARANGA KWA MAPANGA KWA KUCHOSHWA NA UNYWAJI WAKE"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.