Habari za hivi Punde

YULE ASKOFU (MBABE WA IMANI) ALIYEBURUZWA MAHAKAMANI NA WAUMINI WAKE SHINYANGA ASHINDWA KESI

Waumini wa kanisa la EAGT Majengo manispaa ya Shinyanga wakimshangilia mchungaji wao David Mabushi baada ya kushinda kesi ndogo kupinga kuvuliwa uongozi wake ndani ya kanisa hilo.Kesi hiyo ilifunguliwa na waumini wa kanisa hilo wakishirikiana na mchungaji huyo dhidi ya kumpinga askofu wa kanda ya magharibi Rafael Machimu ambaye aliwafukuza wachungaji wanane na kulaumiwa na waumini ambapo kesi hiyo iliendeshwa mahakama ya wilaya shinyanga chini ya hakimu Thomson Mtani ikiwa kesi ndogo imekwisha na kesi ya msingi itaanza kusikilizwa tarehe 29/septemba mwaka huu na kesi ndogo imekwisha tolewa maamuzi kuwa mchungaji huyo aendelee na kazi yake kama kawaida. 

Aliyevaa suti ya kijivu ndiyo askofu wa kanda Rafael Machimu aliyefikishwa mahakamani kwa kosa la kufukuza wachungaji kinyume na katiba ya kanisa kwa maslahi yake binafsi,na hapo katika picha akiwa na wapambe wake akitoka mahakamani .

Waumini wa kanisa la EAGT wakiwa wamembeba mchungaji wao David Mabushi baada ya kuruhusiwa na mahakama kuendelea na uchungaji wa kondoo wa mungu mpaka pale kesi yake ya msingi itakaposikilizwa tena,hapo pichani wakiwa nje ya kanisa baada ya kutoka mahakamani. 

Hapo waumini wakimpokea mchungaji wakati akitoka mahakamani na kuelekea kanisani.


wakiendelea kuchangilia kwa kushinda kesi ndogo.


Waumini wa kanisa la EAGT wakitoka nje ya mahakama ya wilaya ya Shinyanga huku wakiwa na nyuso za furaha baada ya mchungaji wao kuruhusiwa kuendelea na shughuli za uchungaji mpaka pale kesi ya msingi itakapo malizika.

Furaha ikiendelea
Umati wa waumini uliokuwa ukisubiria nje ya mahakama .
Huyu Askofu Rafael Machimu akituhumiwa kwa kuchukua maamuzi yake bila kufutata katiba ya EAGT na kuwafukuza wachungaji ambapo ndio alikuwa akienda mahakamani kwa furahama.

waumini wasema ushindi katiba lazima ifuatwe.

Askofu Machimu akiwa na mke wake mwenye nguo za rangi ya njano na bluu pamoja na wapambe wake akiwa nje ya mahakama ya wilaya siku ya jumatatu wakisubiri shauri dogo nje ya mahakama ya wilaya ya Shinyanga mwanzoni mwa wiki hii.-Picha zote na Chibura Makorongo-Shinyanga

0 Response to "YULE ASKOFU (MBABE WA IMANI) ALIYEBURUZWA MAHAKAMANI NA WAUMINI WAKE SHINYANGA ASHINDWA KESI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.