Habari za hivi Punde

WAUMINI WA KANISA LA EAGT WAANDAMANA KUMKATAA ASKOFU WA KANISA HILO.

ASKOFU  wa kanisa  la EAGT kanda ya magharibi Rafael  Machimu  amefikishwa mahakamani  na waumini wa kanisa hilo kwa kitendo cha  kumpinga  kumfukuza  mchungaji wao  David Mabushi  bila kutenda kosa lolote jambo ambalo walilieleza ni  kwenda  kinyume na taratibu.

Waumini hao wakizungumza kwa nyakati tofauti na waandishi wa habari walisema wameamua kumfikisha mahakamani Askofu huyo wakipinga kitendo cha  mchungaji wao na kudai kuwa hakuna kipengele kilichoainishwa cha kumwondoa mchungaji bila kosa.

“Tumeamua kumfikisha mahakamani askofu Machimu kwa kumwandikia barua ya kumfukuza mchungaji wetu aondoke katika kanisa letu  hivyo tumepinga na hatujafurahishwa na kitendo hicho ndio maana tukaenda ngazi ya mahakama ili ikaamue”walisema waumini hao ambao waliomba majina yao yahifadhiwe’alisema mmoja wa waumini  wa kanisa hilo.


Walisema kanisa hilo lilianzishwa mwaka 1992 likiwa chini ya mchungaji John Chambi ambaye aliondolewa na uongozi wa jimbo la Shinyanga akiwepo mchungaji Rafael Machimu ambaye wakati huo alikuwa katibu wa jimbo hilo.

Waumini hao walisema toka mwaka huo waliendelea kuabudu bila mchungaji hadi mwaka 1999 kanisa hilo lilipelekewa mchungaji Mothes Kuzenza ambaye kwa sasa ni marehemu naye aliondolewa mwaka 2003 katika mazingira ya kutatanisha.

Walisema walivyofuatilia waligundua kuwa ameondolewa kupitia mkono wa Askofu Machimu ambaye wakati huo alikuwa katibu wa kanda hivyo walidai wamechoka kuondolewa  wachungaji wao mara kwa mara.

“Kwa kweli tumechoka kuondolewa ondolewa wachungaji mara kwa mara tumeamua sasa kwenda katika ngazi ya mahakama tuone kama mchungaji wetu Mabushi kama atakuwa na makosa ya kuondolewa katika kanisa la majengo”alisema mmoja wa waumini wa kanisa hilo.

“Sisi ndiyo waumini wa hilo kanisa na ni waumini wa miaka mingi hakuna mali ya EAGT hata bati moja haijaleta mali iliyopo humo ni mali ya waumini lakini kusema aondoke mchungaji aache mali ya EAGT kanisa hilo ni mali ya waumini”aliongeza.

Aidha kesi hiyo ilianza kutajwa tarehe  4 Agosti mwaka huu  katika mahakama ya hakimu mkazi wa mkoa na mara ya pili ilisikilizwa  14 Agosti , ikiwa  iliahilishwa kusikilizwa kwa sababu wakili wa mshitakiwa aliiomba mahakama iahirishe kusikilizwa kutokana na kutoelewa kina cha kesi hiyo hivyo inatarajiwa kusikilizwa tarehe Agost 25 mwaka huu.

 

0 Response to "WAUMINI WA KANISA LA EAGT WAANDAMANA KUMKATAA ASKOFU WA KANISA HILO."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.