Habari za hivi Punde

WATOTO WENYE ULEMAVU WA NGOZI WAONGEZEKA KWA KASI KITUO CHA BUHANGIJA KWA HOFU.

Meya  wa manispaa ya Shinyanga  Gullamu Hafidh Mkadamu akiwa meza kuu na   msimamizi ambaye ni mwalimu Peter Ajali wa shule hiyo akikabishiwa fimbo nyeupe 11 za watoto wasioona huku akielezwa wimbi la kuongezeka kwa watoto wenye ulemavu wa ngozi kila siku watoto watatu mpaka wanne.
MKAMA SHAKENGWA  NI KIONGOZI KATIKA KITUO CHA KULELEA WATOTO WENYE  ULEMAVU MBALIMBALI CHA BUHANGIJA   WAKIWEMO ALBINO.  WATOTO wenye ulemavu  wa ngozi  katika kituo maalumu cha kulea  watoto hao Buhangija manispaa ya Shinyanga ,wamezidi kuongezeka kituoni hapo  kutokana na wimbi la mauaji y a albino  kuibuka tena na kufikia watoto zaidi ya  100  kupelekwa hapo kutoka maeneo mbalimbali kwa hofu ya kuuwawa na kufanyiwa  ukatili.

Pia  watoto wengi wametoka kwenye  mikoa ya Tabora,Simiyu na Mwanza ikiwa  watoto wa kike  98 na  wakiume 96 , baada ya mauaji hayo kuibuka  tena tangu kwenye  mwezi mei mwaka huu kwa kuuwawa mwanamke mmoja huko mkoani Simiyu na mkoani Tabora  watu wawili  kuuwawa kwa kipindi kifupi,ambapo  kila siku watoto watatu mpaka wanne wanaletwa kituoni hapo.

Wakizungumza na waandishi wa habari kituoni hapo wakati wa hafla fupi ya kukabidhi misaada iliyotolewa na wadau mbalimbali wa maendeleo, kupitia harambee iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali Easy flex la mjini Shinyanga kwa ajili ya kusaidia watoto hao huku mwalimu mkuu wa kituo hicho Peter Ajali akieleza changamoto  za ukosefu wa  sehemu ya malazi pia.

Baadhi ya watoto wa kituo hicho  wanaosoma shule ya msingi Buhangija darasa la saba Rehema Masunga,Mkama Shakengwa na D walisema nchi ya Tanzania inasifika kwa kuwa na amani lakini sasa hali inaelekea kuwa mbaya kutokana na baadhi ya watu kuwa na roho za kikatili na kuuwa binadamu kama wanyama .

“Inasikitisha sana kuibuka tena mauaji ya albino tuliona kwenye vyombo vya habari watu wamekatwa mkono,naiomba jamii iwapuuze waganga wa kienyeji maana ndiyo wanachangia, tumuamini mungu atatuepusha na unyama huu wa kikatili”alisema Daniel Limbu.

Naye mwalimu mkuu wa shule hiyo ambaye pia ni msimamizi wa kituo hicho Peter Ajali,alisema kufutia kutokea kwa matukio mawili ya albino kukatwa viungo vyao vya mwili mkoani Tabora na mmoja Bariadi kuuawa  matukio hayo yamesababisha kuongezeka idadi ya watoto kituoni hapo hivyo kuwa na msongamano mkubwa.

Akizunguma kwenye hafla hiyo meya wa manispaa ya Shinyanga Gulamu Hafidhi aliitaka jamii kuwa na utamaduni wa kusaidia kituo hicho,badala ya kutegemea msaada kutoka kwa wafadhili huku akisisitiza mikoa yote iliyopeleka watoto kutoa michango itakayosaidia kukidhi mahitaji na kuwaomba kuielimisha jamii umuhimu wa kusaidia.

Awali mkurugenzi mtendaji wa Easy flex production Happness Kihama alisema changamoto kubwa iliyopo ni uelewa mdogo kwa jamii ,juu ya kusaidia vituo hivyo vyenye mahitaji maalumu wazee na walemavu kutokana na kukabiliwa na changamoto mbalimbali ,ikiwa ni pamoja na uchakavu wa majengo,chakula na malazi.


0 Response to "WATOTO WENYE ULEMAVU WA NGOZI WAONGEZEKA KWA KASI KITUO CHA BUHANGIJA KWA HOFU."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.