Habari za hivi Punde

SHULE YA MSINGI BUGARAMA ILIYOPO HALMASHAURI YA MSALALA WILAYANI KAHAMA INACHANGAMOTO YA MRUNDIKANO WA WANAFUNZI IKIWA DARASA MOJA NI WANAFUNZI 70 HADI 80.


Wanafunzi wa shule ya msingi wakisoma katika mrundikano ambapo walimu wanashindwa kufundisha.


SHULE  ya msingi   iliyopo kwenye   kijiji  na kata ya  Bugarama katika   halmashauri  ya Msalala  wilayani Kahama mkoani Shinyanga  inakabiliwa na changamoto ya mrundikano wa wananfunzi  madarasani ambao umesababishwa na  baadhi  ya vijiji  vya jirani kukosa shule.
  Ikiwa shule hiyo ina jumla ya wanafunzi zaidi ya 1400, vyumba vya madarasa 20, kwa darasa moja  linawanafunzi  70 hadi 80,walimu 32 huku ikikabiliwa  na uhaba wa  nyumba za walimu kwani zilizopo ni nyumba nne pekee.
Waandishi wa habari walitembelea  kijiji hicho huku baadhi ya wananchi wakieleza changamoto ya wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo kuwa  baadhi ya vijiji viwili vinategemea  watoto wao wasome humo kutokana na  maeneo hayo kukosa shule za msingi,ambapo mwalimu mkuu wa shule  Simoni Lasana  alisema hiyo yote inasabaishwa na   vijiji hivyo kuwa na mgodi ambao unafanya  kuwa na mwingiliano wa watu kila siku.
“Mwingiliano  wa watu  sababu ya mgodi wa kakola  ndio umeleta idadi ya kuwa na wanafunzi wengi ,kwani vijiji vingine havina shule kutokana na mwaka 2009  kata ya Bugarama ilizalisha vijiji vitatu ambavyo ni  Igudeja, Bunango na Bugarama , watoto kutegemea  shule hiyo  ikiwa jumla ya wanafunzi ni zaidi ya 1400 huku darasa moja likiwa  na wanafunzi  70 hadi 80”alisema  mwalimu mkuu Lasana.
Pia  alisema kumekuwepo na changamoto ya uhaba wa ofisi   ikiwa darasa moja limegeuzwa kuwa ofisi, nyumba za walimu zilizopo ni nyumba nne pekee huku walimu wakiwa  zaidi ya 30  na mamboma  tisa  ya nyumba za walimu tayari yamekwisha jengwa  ila bado hayajapata wa kusaidia kukamilisha.
Mwenyekiti wa  serikali ya kijiji  cha Bunango Iddi  Binki alisema kuwa kijiji chake kimekamilisha ujenzi wa  madarasa matatu  bado ukosefu wa choo ndio tatizo pindi itakapo kamilika  kunategemewa kuwagawa wanafunzi wengine katika shule hiyo ili kuweza kupunguza msongamano.
Mratibu  wa elimu katika  kata hiyo  Stanley  Mduta alisema kuwa  changamoto hiyo ipo  ila mikakati ya vijiji vilivyoanzishwa  kujenga shule  vimeanza kutekeleza ikiwemo kijiji cha  Bunango kimekamilisha madarasa matatu  lengo kutaka kuwagawa wanafunzi hao,sababu ya kuwepo kwa wanafunzi wengi ni mwingiliano wa watu kwenye mdodi wa dhahabu  wa Bulyanhulu.
Naye mkurugenzi wa halmashauri hiyo Patrick  Kalangwa alisema kuwa  changamoto hiyo ni kweli  kwenye baadhi ya shule ikiwemo hiyo, ikiwa zimeagizwa kamati  za shule kuhamasisha ujenzi wa maboma  na  mgodi wa dhahabu wa  Bulyanhulu  upo tayari kukamilisha maboma hayo kwa mujibu wa mkataba  na mahusiano yaliyopo katika kuondoa changamoto zinazowakabili wananchi


0 Response to "SHULE YA MSINGI BUGARAMA ILIYOPO HALMASHAURI YA MSALALA WILAYANI KAHAMA INACHANGAMOTO YA MRUNDIKANO WA WANAFUNZI IKIWA DARASA MOJA NI WANAFUNZI 70 HADI 80."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.