Habari za hivi Punde

SERIKALI YASHAURIWA KUWEKA MIKAKATI JUU YA UDHIBITI WA UGONJWA WA INI AMBAO UMEANZA KUWA TISHIO.


Waziri wa afya   na ustawi wa jamii Dkt  Seif  Rashid.
SERIKALI  imeshauriwa kuweka mikakati ya kupambana na ugonjwa wa homa ya ini sambamba na kutoa elimu kwa jamii  ambao umeanza kuonekana ni tishio hapa nchini ili kunusuru afya za wananchi.


Ugonjwa huo  umeonekana  kwenda sanjari na maambukizi ya virusi vya ukimwi  ikiwa kampeni inatakiwa wananchi kuelewesha juu ya kujikinga kwake na madhala yake kama inavyo fanya kwa magonjwa mengine.

Ushauri huo umetolewa na kaimu mganga wa Hosptali ya wilaya ya Kahama Dkt  Deo Nyaga  alipokuwa akiongea na mwandishi wa habari hospitalini hapo huku akieleza   kuwa kugundulika kwa ugonjwa huo wa ini nipale wanapochukua vipimo vya vvu kwa wale wanaojitolea damu kwa ndugu zao.

“ugonjwa huu tumekuwa tukiuona tunapo chukua damu kwa watu wanao kuja kujitolea au wanao tolea ndugu zao na kugundua kuwa licha  maambukizi ya ukimwi  tumegundua waliowengi  bado  wanatatizo la ugonjwa wa  ini  hapo baadaye litakuwa tishio , hivyo serikali inatakiwa  ichukue hatua za haraka wananchi kupatiwa elimu’ alisema dkt Nyaga.

Aidha changamoto inayoikabiri  Hosptali hiyo ni mrundikano wa wagonjwa kitendo ambacho wauguzi pamoja na madaktari hawatoshi licha ya jitihada za serikali kujenga vituo vingi  maeneo ya vijijini ikiwemo kuna upungufu wa watumishi ndio maana wagonjwa wengi hukimbilia  hospitali ya wilaya zaidi.

Katika tuhuma za uuzwaji wa damu hosptalini hapo alisema kumekuwa na mawazo potofu kwa baadhi ya watu kwani utaratibu ni kuwa anapo letwa mgonjwa ana tatizo hilo ndugu zake huambiwa watafute mtu wa kumtolea damu na anapo patikana huwekewa damu iliyoko kwenye  kiba na hiyo iliyochukuliwa   huwa ni bahati nasibu kama itakutwa ni salama.

Pia aliobgeza kuwa  wengine wanapo ambiwa watafute ndugu na kukosa huenda mjini kutafuta watu wasio wajua kwa makubaliano ya malipo na wanapo fika kazi  ya wao ni kutoa damu tu si vinginevyo.


0 Response to "SERIKALI YASHAURIWA KUWEKA MIKAKATI JUU YA UDHIBITI WA UGONJWA WA INI AMBAO UMEANZA KUWA TISHIO."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.