Habari za hivi Punde

AZIMIO LIMEPISHWA USAFIRI WA DALADALA KUONDOLEWA MANISPAA YA SHINYANGA KUTOKANA NA BAADHI YA MADREVA KUFANYA VITENDO VYA KIKATILI KWA WATOTO IKIWEMO UBAKAJI NA KUWATOBOA MACHO.


huyu ni  naibu mstahiki meya wa manispaa ya Shinyanga David Nkulila.
BARAZA la madiwani  manispaa  ya  Shinyanga  limeazimia  kuziondoa  daladala zote za baiskeli  kutokana na  baadhi ya madreva wake  kujihusisha na kufanya vitendo vya ukatili dhidi ya watoto kwa kuwabaka na kuwatoboa macho hali ambayo imefanya jamii kuingiwa na hofu  kubwa dhidi yao.

Wakiongea katika baraza hilo lililofanyika kwenye ukumbi wa mkoa baada ya  mchumi wa manispaa hiyo Christopher Nyarubamba alisoma  taarifa ya  maazimio  yaliyoafikiwa  na madiwani kuwa daladala zote za baiskeli hazitakiwi ,  ambapo zimelekezwa ziwe  kando ya mji kwa kusajiliwa na kupewa vitambulisho ikiwa utekelezaji wake unatakiwa kuanza mara moja.
Nyarubamba  katika taarifa yake alisema kuwa  waendesha daladala za baiskeli wanatakiwa kuondoka kutokana na kushamiri kwa vitendo vya kikatili dhidi ya watoto,huku baadhi ya madiwani akiwemo diwani viti maalumu Shella Mshandete  kuunga mkono azimio hilo na kueleza kuwa  wananchi wa manispaa wanatakiwa kubadilika kama maeneo mengine mbona  kuna daladala za magari  hakuna baiskeli wao wanashindwa nini?.
Pia diwani  vitimaalumu  (chadema)  Siri Yasin alisema kuwa  hakuta wezekana kuwafukuza  waendesha  daladala za baiskeli bila kufahamu  mbadala wake,hivyo inatakiwa usafiri upatikane ndipo zoezi la kuwaondoa lianze   bila hivyo jamii haitaelewa kwani wamezoea usafiri huo kuwakatisha ghafla italeta tatizo pia.
“Jamani  tunapoanza kuziondoa daladala za baiskeli tufahamu  wazi kwamba tutawapa shida wananchi  waliozoea usafiri huo,kinachotakiwa kuwepo na mbadala  wake  mimi sipingi kuwa wasiondolewa kwani vitendo vya ukatili kwa watoto manispaa vimezidi kuongezeka ukiangalia chanzo ni madreva wa daladala  wenye kwenda kwa waganga wa kienyeji kutafuta utajiri wa haraka”alisema  Yasini.

Katibu tawala wa wilaya Boniface Chambi  alisema kuwa  daladala za gari zilikuwepo  na uzinduzi ulifanywa na mkuu wa mkoa Ally Rufunga  lakini cha kushangaza  watu walikuwa hawazipandi  huku wakiwakatisha tamaa wenye daladala hizo matokeo yake zikasitishwa mpaka leo hii  kunaonekana daladala za baiskeli pekee.
Kwa upande wake naibu mstahiki meya  manispaa hiyo David Nkulila alisema kuwa   daladala  za baiskeli ziondolewe kama lilivyopitishwa azimio,pia aliwanyooshea kidole  baadhi ya maaskari kukamata magari ya abiria hovyo kwa mitazamo yao ya kimaslahi hivyo kwa hilo halitavumiliwa hata kidogo inatakiwa wajirekebishe kwenye utendaji wao wa kazi.


0 Response to "AZIMIO LIMEPISHWA USAFIRI WA DALADALA KUONDOLEWA MANISPAA YA SHINYANGA KUTOKANA NA BAADHI YA MADREVA KUFANYA VITENDO VYA KIKATILI KWA WATOTO IKIWEMO UBAKAJI NA KUWATOBOA MACHO. "

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.