Habari za hivi Punde

TIMU YA STENDI UNITED NA POLISI MARA ZALETA KIZAA ZAA UWANJA WA KAMBARAGE MKOANI SHINYANGA

BAADHI ya  mashabiki  wa timu  ya mpira wa miguu manispaa ya shinyanga akiwemo naibu waziri wa nishati na madini Steven Masele kunusurika  na wengine  kujeruhiwa vibaya  sehemu mbalimbali za miili yao kutokana na  vurugu zilizozuka  ndani ya uwanja wa Kambarage  ambapo jeshi la polisi lilianza kurusha mabomu ya machozi .
Mabomu hayo yaliweza kuleta madhara kwa mashabiki  ambapo  mama mwenye ujauzito wa miezi nane aliyefahamika kwa jina la Johari Abdallah (23) mkazi wa ngokolo amelazwa kwa presha  katika hospitali ya mkoa  na mwamuzi  Steven Lutaselwa aliyekuwa  jukwaani akiangalia mpira alijeruhiwa vibaya  sehemu za makalio na hali yake bado ni mbaya yuko chumba mahututi.
Katika mechi iliyokuwa ikichezwa na timu za   Stand  united  ya Shinyanga  pamoja na timu ya Polisi Mara zilikuwa zikiminyana  siku ya jumamosi katika uwanja wa kambarage huku mgeni rasmi akiwa naibu waziri huyo ambaye pia ni  mbunge wa jimbo la Shinyanga  mjini naye alipigwa mabomu mawili ya machozi yaliyotupiwa mezani na kuamuru kwenda kujificha kwenye chumba cha mazoezi   (GYM)
Ilionyesha kuwa mabomu hayo yalipigwa  baada ya mchezo kumalizika huku stendi  united ikishinda kwa goli moja kwa bila katika  mchezo huo,ambapo mwamuzi  aliyekuwa akichezesha pembeni  alivamiwa na  kiongozi  kutoka timu ya polisi Mara kutaka kumpiga huku polisi waliokuwepo ndani ya uwanja huo wakitazama bila kwenda kutoa msaada wowote.
Hata hivyo vurugu zilianza baada ya   kocha msaidizi wa timu  ya Polisi Mara kwenda kupeana mkono na kocha wa timu ya  Stend united  ndipo  alipofika eneo la kikosi cha timu hiyo   kabla ya kupeana  mkono alimnasa kibao  kocha wa timu ya stend united ambapo  kiongozi wa nidhamu  wa timu hiyo Said Mponda alipokwenda kuamua  alianza kushambuliwa na polisi.
Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu (Shirefa)  mkoani Shinyanga  Benesta Lugolla alisikitishwa na  kitendo cha polisi kutumia nguvu kubwa  kuchambulia mashabiki waliokuwa  wamekaa jukwaa kuu  akiwemo na mgeni rasmi kitendo ambacho kimeonekana ni udhalilishaji hata kwa naibu waziri huyo ikiwa chama kiliomba askari wachache  cha kushangaza waliokuja ni wengi.
Baada ya kuhojiwa  na waandishi wa habari  naibu waziri  Masele alieleza kuwa  aliiomba shirikisho la mpira wa miguu nchini  (TFF) kuangalia upya timu za majeshi  hasa polisi kwani wamekuwa chanzo cha matatizo  katika viwanja vingi ,pia wamekuwa wakilindana na kutotaka kushindwa  inaonekana mpango huu ulikuwa  umesukwa muda mrefu..
 
 

0 Response to "TIMU YA STENDI UNITED NA POLISI MARA ZALETA KIZAA ZAA UWANJA WA KAMBARAGE MKOANI SHINYANGA "

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.