Habari za hivi Punde

WAFANYABIASHARA WALALAMIKIWA KUWA CHANZO CHA UCHAFU WA MITARO NA MAKALVAT



WAFANYABIASHARA   mkoani  Shinyanga wamelalamikiwa kuwa chanzo cha kuchafua mitaro na  makalvati  ikiwemo mama lishe  kumwaga maji machafu   hali ambayo imesababisha mitaro hiyo kuziba  na kufanya   wakala wa barabara  tanroad  kuingia  gharama  kubwa ya kuzibua na  kuisafisha .

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake  meneja wa  Tanroad mkoa wa Shinyanga  Philip Witonde  amesema   kuwa  wafanyabishara wanapouza bidhaa zao mabaki  ambayo  ni uchafu hutupwa katika  mitaro  huku mama lishe nao humwaga maji machafu   hali inayopelekea mitaro hiyo kuziba kwa haraka.


Witonde amesema  kuwa   wafanyabishara   wamekuwa ni chanzo cha   kuwepo  kwa  uchafu  katika mitaro kwani hufanya biashara zao   kando ya barabara na mabaki  huhifadhi katika mitaro au makalvati  isitoshe mama lishe  nao  hudiriki kumwaga maji machafu  hali ambayo inawafanya  wakala wa barabara kutumia gharama kubwa kuzibua  na kuisafisha.

Witonde amesema  Suala la wanaosafisha   barabara za manispaa  waliokuwa wanafanya usafi  kwakutumia mafagio na kusukuma michanga katika  mitaro hilo waliliona na kumwandikia barua  mkurugenzi   wa manispaa ya shinyanga  kuwa mchanga sio kuskumwa ndani ya mitaro bali wawe na eneo maalumu ya kutunza michanga hiyo.

Baadhi ya wananchi wamekuwa  sio watunzaji wa mazingira amesema   mara nyingi kumekuwa  wakiweka  uchafu wa aina mbalimbali katika Kalvat na mitaro ,kwa kuona   chupa za plastiki  ndani yake kuna haja ndogo,mifuko ya plasiti yenye kinyesi  pamoja na kuchora au kuandika  kwa kuchafua kuta za mitaro.

Witonde amesema  Suala la wanaosafisha   barabara za manispaa  waliokuwa wanafanya usafi  kwakutumia mafagio na kusukuma michanga katika  mitaro hilo waliliona na kumwandikia barua  mkurugenzi   kuwa mchanga sio kuskumwa ndani ya mitaro bali wawe na eneo maalumu ya kutunza michanga hiyo.

Baadhi ya wafanyabiashara  wamekiri  kumwaga maji machafu katika mitaro ambapo wamesema kuwa   kuna wengine sio wastarabu  jambo ambalo wamekuwa wakiambiwa kila siku  usafi wa mazingira kwa kuwa na sehemu ya kuhifadhia maji machafu na taka ngumu pia kuondokana na magonjwa ya mlipuko.

0 Response to "WAFANYABIASHARA WALALAMIKIWA KUWA CHANZO CHA UCHAFU WA MITARO NA MAKALVAT"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.