Habari za hivi Punde

WATU WATATU WAMEFARIKI DUNIA KATIKA MAPIGANO KATI YA WAKULIMA NA WAFUGAJI WILAYA ZA KISHAPU NA IGUNGA





WATU watatu ambao majina yao hawajafahamika  wamefariki dunia huku  mfugaji  Gilijisiji Gilawida ambaye alichomwa mkuki na kumjeruhi  vibaya  sehemu za mwili wake  katika mapigano ya wakulima na wafugaji  huko katika kijiji cha  Isakamaliwa  kilichopo mpakani mwa mkoa wa Shinyanga  na Tabora  ambapo mapigano hayo  yalisababishwa na  kugombea  mipaka ya malisho.

Hata hivyo kwa upande wa kata ya Magalata  wilayani Kishapu mkoani Shinyanga waliopo wafugaji wengi  wa kabila la kitaturu   walinyang’anywa mifugo yao zaidi ya 3000 na wakulima kutoka kijiji hicho kilichopo wilayani Igunga  mkoani Tabora huku ikionekana uchochezi huo kufanywa na wafanyabiashara.


Wakiongea na  mwandishi wa habari  katika eneo hilo  baadhi ya wafugaji walisema kuwa  chokochoko hizo zimetokana na wakulima kulima mazao  maeneo yote hiyo kusababisha  wao kukosa maeneo ya malisho,na wanapo kwenda kulisha mifugo  mara nyingine huwanyang’anya mifugo yao kwa nguvu jambo ambalo hupingana nalo.

Walisema tayari ng’ombe zaidi ya 3000  wameswagwa na kupelekwa wilaya ya Igunga jambo ambalo wafugaji hawakukubali hivyo  walianzisha mapigano yaliyosababisha baadhi ya  wafugaji kujeruhiwa huku wengine watatu wakipoteza maisha na mmoja yuko mahututi kwa kujeruhiwa vibaya.

Mmoja wa wafugaji  hao Ndelanha Mahona   alisema kuwa    mifugo yake imechukuliwa na wakulima na kuondoka nao wilaya ya Igunga sababu wanayodai ni mifugo kuingia katika mashamba yao  na kula mazao hali ambayo inaonyesha kuwa ni kuwanyanyasa ikiwa eneo hilo wamekuwa wakilitumia miaka yote.

Hata hivyo mwenyekiti wa hal mashauri hiyo  Justin Sheka alisema kuwa  mapigano hayo yametokea hali ambayo imehatarisha amani kwa wafugaji ikiwa aliwataja walionyang’anywa mifugo hiyo kuwa ni  Ndelanha Mahona,Mbuta Madila Silag’wan Hendeka, Gidi  Babashi, Mfano Gilawida ,Gilajuli Dudula,Magai Dudula,Gishauli Udadi na aliyejeruhiwa ni  Gilijisiji  Gilawida.

Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Kishapu  Shija Ntelezu alisikitishwa na kitendo hicho huku akiitaka serikali  kuthibiti uchungaji holela na kulipatia ufumbuzi suala  la mbuga hizo mbili kwani mbuga ya Magalata ilikuwa ni eneo kwaajili ya malisho lakini wakulima wameliingilia  na kufanya shughuli za kilimo holela.

“Serikali lazima ifanye mikakati ya kupata ufumbuzi wa kina kwenye suala hili kwa watu wameshaanza kuuana hovyo, wadhibiti  uchungaji na ukulima holela ikiwa eneo la Magalata lilitengwa kwaajili ya ufugaji  hivyo liwekewe uzio ,sasa watu  wanafanya shughuli za kilimo bila utaratibu wafugaji wanakosa sehemu za malisho  ndio sababu ya mapigano huku wafanyabishara wakiwa chanzo chanzo”alisema Ntelezu.

Naye mkuu wa wilaya ya Kishapu  Wilson Nkhambaku alisema kuwa  kweli mapigano hayo  yalitokea tangu juzi  katika eneo la Magogo linalotenganisha  wilaya ya Igunga na Kihspau  ikiwa mtu mmoja alifariki dunia  wa kutoka wilaya ya Igunga  huku wafugaji kutoka Kishapu wakinyang’anywa mifugo ya zaidi ya 3000 kupelekwa Igunga.

“Tulikaa kamati ya ulinzi na usalama kujadiliana suala hilo na kwenda katika  eneo la mpakani kwenda kuwasilikiza  lakini siku ilivyofuata  ilipata tena taarifa kuwa mapigano yanaendelea na tayari baadhi ya watu wamejeruhiwa na wengine kuendelea kupoteza maisha”alisema  Nkhambaku.

0 Response to "WATU WATATU WAMEFARIKI DUNIA KATIKA MAPIGANO KATI YA WAKULIMA NA WAFUGAJI WILAYA ZA KISHAPU NA IGUNGA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.