Na Anitha Jonas, MAELEZO-DSM
SERIKALI imesema kuwa mradi wa gasi kutoka Mtwara hadi katika kituo cha Kinyerezi jijini Dar es Salaam unatarajia kukamilika mwishoni mwa mwaka huu (2014) na kuanza majaribio Januari, 2015.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Bw. Eliakim Maswi wakati wa ziara ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa mitambo ya gesi katika eneo la Kinyerezi.
Katibu Mkuu huyo alisema hadi hivi sasa mradi huo wa gesi umekamilika kwa zaidi ya asilimia 70.(Martha Magessa)
Aliongeza
kuwa hivi sasa uzalishaji wa umeme katika Shirika la TANESCO
unaigharimu Serikali shilingi1.6 trilioni kwa mwaka, hivyo baada ya
mradi huo kukamilika, serikali itaokoa kiasi hicho cha fedha na
kuzielekeza katika miradi mingine ya jamii.
Mradi wa
gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam utagharimu dola za Kimarekani
shilingi 183 millioni, hadi sasa, serikali imekwishalipa Dola milioni
139 bado dola 44 millioni.
Naye
Mhandisi wa mradi huo Bw. Simon Gilima, alisema kuwa jumla ya Megawatt
150 zitazalishwa na kuingizwa kwenye gridi ya taifa na kusaidia
uzalishaji wa umeme kwa bei nafuu.
Mmoja wa
wadau wa maendeleo nchini ambaye pia ni Mkurugenzi wa UN nchini Bw.
Philippe Dongier alielezea kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa mradi
huo ambao pia alisema utaongeza ajira nchini na pato la taifa.
Aliishauri Seriakli ya Tanzania kuendelea kubuni miradi mingine itakayosaidia kupunguza tatizo la ajira nchini.
Vile vile aliiomba Serikali kuwa makini na masuala ya uwekezaji ili kulinda na kusimamia Sera na matakwa ya nchi.
Ziara
hiyo ya Katibu Mkuu huyo kwenye eneo hilo ililenga kuangalia maendeleo
ya ujenzi wa mradi huo ambapo pia iliwashirikisha wadau mbalimbali wa
maendeleo nchini ikiwemo Benki ya Dunia, JICA, Umoja wa Mataifa (UN) na
TPDC.
0 Response to "MRADI WA GESI WA MTWARA UNATARAJIA KUANZA MAJARIBIO JIJINI DAR."
Post a Comment