Habari za hivi Punde

MZAZI ANAYEPENDA PESA AMKATAZA MTOTO WAKE ASIFANYE MTIHANI WA DARASA LA SABA KISA AOLEWE.

Katika hali isiyotarajiwa, Athanas Lusesa ambaye ni mzazi wa mwanafunzi anayesoma katika shule ya msingi Ihulike iliyopo katika kata ya Ushirombo Wilaya ya Bukombe mkoni Geita amemkataza binti yake kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi .

Mwanafunzi wa kike aliyezuiwa kufanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi na mzazi wake kwa hofu ya kufaulu na kuharibu mipango ya mzazi wake ya kutaka kumuoza ili apate pesa ya mahari kutoka kwa mwanaume amefahamika kwa jina la Shija Athanasi(14)wa shule hiyo ya msingi Ihulike.

Afisa Elimu msingi Wilaya ya Bukombe Shadrack Kabanga amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kufuatia tukio hilo alikwenda kituo cha polisi Ushirombo na kuchukua askari ambao walimkamata mzazi huyo.

Tayari mzazi huyo anashikiliwa na jeshi hilo kwa mahojiano zaidi na atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Naye mkuu wa wilaya ya Bukombe Amani Mwenegoha amelaani vikali kitendo hicho kilichofanya na mzazi huyo kwa lengo la kujipatia mali na kuahidi kuwashughulikia wazazi wanaozuia jitihada za serikali kuhakikisha mtoto wa kike anapata elimu.

Na Victor Bariety

0 Response to "MZAZI ANAYEPENDA PESA AMKATAZA MTOTO WAKE ASIFANYE MTIHANI WA DARASA LA SABA KISA AOLEWE."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.