Habari za hivi Punde

TIMU YA YANGA YAZIDI KUNG'ARA NI BAADA YA KUIBUKA NA USHINDI MNONO WA MABAO 3-0 DHIDI YA STEND UNITED YA MKOA WA SHINYANGA

http://images.supersport.com/2013/5/Yanga-celebrate-300.jpg 
Bunda la mkosi limeendelea kuiandama Simba baada ya kulazimishwa tena sare ya bao moja kwa moja na maafande wa Prisons katika Uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya wakati mahasimu wao Yanga wakipata ushindi mnnono wa 3-0 dhidi ya Stand United mjini Shinyanga.
 
Yanga imefikisha pointi kumi baada ya kucheza michezo mitano na kuwacha mahasimu wa Simba nyuma kwa pointi tano baada ya kupata sare yake ya  tano kutokana na michezo yake mitano.
Tofauti na furaha na nderemo za Wanajangwani, Simba mambo si shwari, kwani matekeo haya mabaya sana tangu kuanzishwa kwake kwa kuambulia pointi tano kutokana na mechi tano ambayo yanaifanya timu hiyo kupoteza jumla ya pointi kumi tangu kuanza kwa msimu huu wa Vodacom Premier League.
Ilionekana kama Simba ingepata ushindi wake wa kwanza jijini Mbeya baada ya kuongoza kwa kipindi kirefu, lakini ndoto yao ilikatishwa katika dakika za majeruhi baada ya Prisons kusawazisha.
Simba ilipata bao la kuongoza kupitia kwa Mganda Emanuel Okwi kabla ya Prisons kuchomoa dakkika za majeruhi kupitia kwa Hamisi Mahingo.
 
Tofauti na matokeo ya Mbeya, Yanga imeweza kupata ushindi wake wa kwanza mnono.
Mbrazil Geilson Jaja alifungua ukurasa wa mabao katika dakika ya 13 kwa bao ambalo lilidumu hadi mwisho wa kipindi cha kwanza.
 
Kipindi cha pili Yanga iliongeza kasi na kuweza kupata mabao mawili zaidi kupitia kwa Jerryson Tegete katika za 77 na 90.
 
Matokeo mengine ya kushangaza ni kuwa Azam wameonja uchungu wa kufungwa baada ya kuzabwa bao 1 kwa bila na JKT Ruvu katika uwanja wake wa Chamazi.
Bao la Samuel Kamuntu katika dakika ya 44 ndilo lililoizamisha Azam na kuifanya ione adha ya kufungwa kwa mara ya kwanza.
 
Kutoka Mlandizi mkoani Pwani, mwandishi wetu anaripoti kuwa wenyeji Ruvu Shooting imewachapa maafande wa Polisi Morogoro kwa bao moja kwa bila katika mchezo mkali uliojaa upinzani.
 
Alikuwa ni Kassim Daby aliyewainua Ruvu Shooting baada ya kupachika bao la ushindi katika dakika ya 68 baada ya kuunganisha kimiani mpira wa kona iliyopigwa kiustadi na Hamisi Nguya.
Mpira uliimalizika katika dakika 45 za kwanza kwa sare ya kutofungana kabla ya wenyeji kujipatia bao la ushindi dakika 23 baada ya kuanza kwa kipindi cha pili.

0 Response to "TIMU YA YANGA YAZIDI KUNG'ARA NI BAADA YA KUIBUKA NA USHINDI MNONO WA MABAO 3-0 DHIDI YA STEND UNITED YA MKOA WA SHINYANGA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.