Habari za hivi Punde

RC-SIMIYU AMEWATAKA WAKUU WA WILAYA WAPYA KUKOMESHA MAHAKAMA ZA KIMILA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Antony Mtaka amewataka wakuu wa wilaya wapya kuhakikisha wanakomesha  mahakama za kimila maarufu kama  Ndagashida  ambazo zimekuwa zikitoa adhabu kwa watumishi wa umma  wasio na hatia hali inayopelekea kutokea kwa  mauaji , vilema vya maisha sambamba na kuwafirisi mali zao.
 
Akitoa wito huo jana wakati wa kuapishwa  wakuu hao  ,Mtaka alieleza kuwa  ni muhimu kwa wakuu hao kuzingatia suala hilo  katika wilaya zao kwani  limekuwa likionekana  kuwa ni kikwazo kwa watumishi wa umma ambao hawakubaliani na mila zisizokuwa za kwao.
 
 Amesema ni dhahiri kwamba ili mkoa uendelee kuwa na  watumishi  waishio kwa  amani , ni lazima kukomesha Ndagashida ili watu na watumishi waendelee kufurahia kuishi Mkoani Simiyu.
 
Sambamba na hilo Mtaka pia amewasihi wakuu hao wa wilaya kuhamasisha wananchi juu ya utunzaji wa mazingira ambao utaenda pamoja na upandaji wa miti ili kunusuru mkoa kuangamia na kuwa jangwa.
 
Ameeleza kuwa hali ya mazingira  si zuri na kwamba Mkoa unakaribia kugeuka kuwa jangwa   ambapo inaweza kusababisha maisha ya wakazi wa Mkoa kuwa magumu.
 
“hali ya  utunzaji wa mazingira  si nzuri…hivyo ninawaomba waheshimiwa wakuu wa wilaya kuhamasisha watu kupanda miti…hasa kwa kuanzia katika taasisi kwani itasaidia kuondokana na ukame uliotawala ndani ya Mkoa.
 
Aidha  mara baada ya kuapishwa mkuu  wa wilaya ya Meatu Joseph Chilongani amesema kipaumbele kimojawapo ambacho ataanza  kukifanyia kazi  kabla ya  shule za msingi kufunguliwa hapo julai 11, mwaka huu ni kufanya uhakiki wa wanafunzi wote ambao wako katika mpango wa elimu bure kama inavyoelekeza na serikali ya awamu ya tano.
 
Chilongola amesema ni lazimaashughulikie suala la uhakiki wa hao wanafunzi ili isije kuwa kuna wanafunzi hewa ambao hela zao zinatumika na wajanga ndani ya idara ya elimu.
 
Sambamba na hilo ameomba ushirikiano wa karibu kutoka mkurugenzi ,wakuu wa wilaya na watumishi ili waweze kufanya kazi ya kuwaletea wananchi maendeleo.
 
 Jumla ya wakuu wa wilaya watano   wa wilaya  tano za mkoa wa Simiyu wameweza kuapisha leo  na mkuu wa Mkoa wa Simiyu Antony Mtaka ambao ni Joseph Chilongani (Wilaya ya Meatu ,) Tano Mwera (busega), Seif Shekalaghe(Maswa) Benson Kilangi(Itilima)na  Festo Kiswaga (Bariadi)

0 Response to "RC-SIMIYU AMEWATAKA WAKUU WA WILAYA WAPYA KUKOMESHA MAHAKAMA ZA KIMILA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.