Habari za hivi Punde

TATIZO SIO HOSPITALINI BALI BOHARI ZA DAWA HUCHELEWESHA



IMEELEZWA kuwa vifaa tiba na madawa huchelewa kuwafikia katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga  hali ambayo imepelekewa wagonjwa   kupata changamoto ya ukosefu wa dawa hospitalini hapo.

Hayo yameelezwa na mganga mfawithi wa hospital hiyo Dkt    Fredrik Mlekwa  wakati akiongea na waandishi wa habari jana hospitalini  hapo baada ya kupata malalamiko  ya wagonjwa kukosa dawa ikiwemo vifaa tiba.
Hata hivyo  amesema kuwa  katika suala hilo aliiomba Serikali  kuangalia upya utaratibu wake wa kusambaza madawa pamoja na vifaa tiba viweze kufika kwa muda muafaka,
Aidha amesema kuwa   kitengo cha  bohari ya dawa  MSD kilichopewa jukumu la kusambaza  wamekuwa wakichelewa kufikisha na pia kuleta  vifaa  ambavyo hawaku agizwa..
 Amesema  kumekuwa na changamoto nyingi za madawa na vifaa tiba  pamoja na serikali kila baada ya bajeti kupita wizara   hupelekwa fedha  MSD kwa ajili ya  vifaa tiba na madawa ambapo  haviji kwa muda muafaka.
 Akiitupia lawama MSD  anasema kuwa  uwezo wao wakusambaza dawa ni asilimia 25 au 30 na asilimia inayobaki   hununua dawa kutokana na  upatikanaji wa  vyanzo vya Hosptalini hapo.

 Amesema  kutokana na changamoto hizo  viongozi  huandaa  mahitaji na kupeleka mkoani kitengo cha manunuzi kwa ajili ya kutangaza tenda ya mahitaji ya madawa na ndio mzunguko huo hujenga  malalamiko toka kwa wagonjwa  madawa yanapo adimika.


0 Response to "TATIZO SIO HOSPITALINI BALI BOHARI ZA DAWA HUCHELEWESHA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.