Habari za hivi Punde

MADIWANI WAKATAA UTOAJI WA SHILINGI MILLIONI 24 KWENYE KITUO CHA KULELEA WATOTO WENYE ULEMAVU


MADIWANI wa halmashauri ya  manispaa ya Shinyanga  wametaka kuondolewa katika orodha ya kuchangia fedha kituo  maalumu cha   kulelea watoto  wenye ulemavu mbalimbali   Buhangija ikiwa katika mchango huo manispaa imelezwa kuchangia kiasi cha shilingi millioni 24.

 

 Hatua ya kukataa kuchangia imetokana na  kituo hicho kulea watoto wanao toka  maeneo tofauti kama vile mkoa wa Geita,Simiyu, Tabora, Mwanza pamoja na Shinyanga hali ambayo  mikoa hiyo imekuwa haitoi msaada wowote.

 

 Madiwani hao wakiongea katika baraza la madiwani jana  lililofanyika kwenye ukumbi wa mkoa  wamesema  kuwa hawatakuwa tayari kuchangia pesa hizo kutokana na kituo hicho kuwa ndani ya manispaa  na majukumu mengi wamekuwa wakikabiliana nayo,

 

 Naibu mstahiki meya  David Nkulila amesema  kuwa  hali ya kituo hicho  hairidhishi  kutokana na kuachanizwa kwa manispaa pekee kutunza watoto hao  isitoshe imepangiwa  kuchangia shilingi millioni 24 ambapo haiwezekani 

 

 Mkuu wa kituo hicho mwalimu Peter Ajali amesema  kuwa   watoto walipo ni 258 ambapo  walemavu wa ngozi  172,wasioona 48,viziwi  38  ikiwa changamoto kubwa iliyopo ni uhaba wa chakula na deni la shilingi millioni 4.8  kutoka mamlaka ya maji  manispaa (Shuwasa) kudai  kituo hicho.

 

Ambapo suala la deni la maji injinia kutoka shuwasa Slyvesta Malole alieleza madiwani kuwa  deni hilo  linadaiwa tangu mwaka jana  huku akilalamika kutofahamu hali halisi ya maisha ya kituo hicho kwa watoto ikiwa alisisitiza kuwa akaunti inayosoma kwa sasa ibadilishwe na kufahamika na deni hilo lazima lilipwe.

 

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Annarose  Nyamubi alisema kuwa  kwa upande wa wilaya ya Bukombe mkoa wa  Geita kuna watoto zaidi ya 30 hivyo idara ya maendeleo ya jamii wanatakiwa kufanya mawasiliano ili halmashauri ziwatambue watoto wao pia suala la kuletwa watoto wapya kila siku waletwe kwa utaratibu  utakao ridhia pande zote mbili.

 

MWISHO.

 

0 Response to "MADIWANI WAKATAA UTOAJI WA SHILINGI MILLIONI 24 KWENYE KITUO CHA KULELEA WATOTO WENYE ULEMAVU"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.