Habari za hivi Punde

WANAFUNZI WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA WAPATA NAFASI WOTE



MKOA wa Shinyanga umefanikiwa kuingiza kidato cha kwanza wanafunzi wote waliomaliza elimu ya msingi  na kufaulu kwa mwaka jana.

Katika taarifa iliyotolewa  kwa waandishi w a habari jana kaimu afisa elimu wa mkoa wa Shinyanga ambaye ni afisa elimu  ya watu wazima mkoa huo Yohana Mkumbo amesema  kuwa   zaidi ya  wanafunzi 28,000 kati yao  wanafunzi 13604 walifaulu mtihani huo kujiunga na kidato cha kwanza .

Mkumbo amefafanua  kuwa kati ya wanafunzi hao wavulana ni 7460 na wasichana ni 6144 na kuongeza kuwa wilaya ya Kahama inaongoza kwa kufaulisha wanafunzi 3868 ikifiatiwa na wilaya ya halmashauri ya mji wa Kahama iliyofaulisha wanafunzi 2953.

Amesema  katika idadi hiyo   manispaa ya Shinyanga  imefaulisha  wanafunzi 2297, wilaya ya Kishapu wanafunzi 2266 huku wilaya ya Shinyanga ikifaulisha wanafunzi 2220 ambapo mkoa umefanikiwa kuwaingiza kidato cha kwanza wanafunzi wote waliofauli kwa asilimia 100.

Aidha amesema  kuwa licha ya mkoa kujivunia hatua hiyo lakini bado unakabiliwa na changamoto ya mwitikio mdogo wa elimu kwa upande wa wazazi hali inayopelekea baadhi ya wanafunzi kukatisha masomo ambapo jumla ya wanafunzi 458 hawakufanya mtihani huo kutokana na sababu mbalimbali.

Kwa upande wa changamoto ya uhaba wa  maabara kwenye baadhi ya shule  amesema  kuwa mkoa unafanya jitihada za makusudi ili ifikapo mwaka  2015 mkoa uwe umetatua tatizo hilo kwa shule zote za sekondari ambapo  ikiwa mkoa una maabara 59 huku mahitaji halisi ni maabara 347.




0 Response to "WANAFUNZI WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA WAPATA NAFASI WOTE"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.