Habari za hivi Punde

BAADHI YA WAZAZI KATA YA NDEMBEZI WALALAMIKIA UONGOZI WA SHULE



BAADHI  ya wazazi   wa  kata ya Ndembezi manispaa ya Shinyanga  wamelalamikia uongozi wa  shule ya msingi Bugoyi (B)   kwa  kitendo cha  kuchangisha shilingi 10,000  kwaajili ya madawati  pindi wanafunzi  walipokuwa wakiandikishwa darasa la kwanza   miaka mitatu mfululizo   iliyopita  lakini matokeo yake   mpaka sasa bado wakiendelea  kukaa chini.


Wakiongea na  mwandishi wa habari   aliyetembelea katika kata hiyo  walisema kuwa  walimu walitilia mkazo wa utozwaji  wa shilingi 10,000 kwaajili ya mchango wa madawati huku wakidai kuwa kama fedha hizo hazitatolewa  mwanafunzi hataandikishwa shule.


Wazazi hao walisema kuwa kiasi cha fedha walichokuwa wakitozwa kwa kutishiwa watoto wao kutoandikishwa shule  mpaka wawe wamekitoa,  wamesikitishwa kwa kuoana bado wanaendelea kukaa chini  huku fedha hizo wakiwa tayari wamekwisha lipia tangu kuanza kwao darasa la kwanza.


Mmoja wa wazazi hao  Jenipher  Subi alisema kuwa  mtoto wake aliandikishwa darasa la kwanza mwaka 2012  akitoa michango yote iliyokuwa ikihitajika shuleni hapo ikiwemo dawati  
chakushangaza  mwaka huu yuko darasa la tatu  bado anaendelea kukaa chini huku akiutaka uongozi wa shule kutoa ufafanuzi wa kina  ili  kufahamu nini tatizo.


“Kweli inasikitishwa kwa kuona watoto wakiendelea  kukaa chini  wakati wazazi tumelipa, walipokuwa wakiandikishwa darasa la kwanza waliweka msisitizo  mtoto hawezi kuandikishwa mpaka awe amelipa mchangao wa dawati kiasi cha shilingi 10,000  ambapo tulitegemea  wanafuzni watakuwa wakisoma wakiwa wamekaa kwenye madawati hali ambayo imekuwa kinyume sasa tatizo lipo wapi”alisema mzazi huyo.


Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule hiyo Anord Rweshabura  alisema kuwa shule hiyo inajumla ya wanafunzi zaidi ya 900 waliochangia madawati hawafiki 30 ikiwa michango iliyotolewa na wazazi imepelekwa kukarabati madawati yaliyokuwepo ambapo wanaokalia  madawati hayo ni darasa la kwanza, darasa la pili na darasa la saba madarasa yaliyobaki wanakaa chini. 


Naye mratibu wa elimu kata ya Ndembezi  Bulugu Selemani alisema kuwa  changamoto kubwa iliyopo baadhi ya wazazi wamekuwa hawatoi michango hiyo kama  wanavyokubaliana kwenye vikao,utakuta waliochanga hawafiki zaidi ya 50 ikiwa dawati moja linauzwa  shilingi 70,000 mpaka  shilingi 80,000 na fedha hizo hazitolewi kwa wakati ndio tatizo  wanafunzi kuendelea kukaa chini.


Diwani wa kata ya hiyo David Nkulila ambaye pia ni naibu meya wa manispaa ya Shinyanga alisema kuwa malalamiko ya  baadhi ya wazazi yamemfikia kuhusiana na tatizo hilo ikiwa tayari ameweka mikakati ya kuitisha mkutano wa hadhara ili kuweza kukutana kwa pande zote  kwa mwenye hoja na kujibiwa lengo kuweza kupata ufumbuzi wa nini kifanyike.




0 Response to "BAADHI YA WAZAZI KATA YA NDEMBEZI WALALAMIKIA UONGOZI WA SHULE"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.