Habari za hivi Punde

WAZAZI NA WALEZI WAKABIDHIWA MADAWATI KWA PESA WALIZOKUWA WAMECHANGA.





Na  Kareny  Masasy
Shinyanga.

WAZAZI na walezi wanaowasomesha watoto wao katika shule ya msingi Bugoyi (A) iliyopo manispaa ya  shinyanga  wamekabidhi jumla ya madawati sabini na mbili kwa ajili ya kuondokana na changamoto ya   kusoma na kuandika  huku wakiwa wamekaa chini na kuwajengea  msingi wa kupata elimu bora.



 Zoezi hilo limefanyika jana wakati mwenyekiti wa kamati ya shule Peter Sangwa akikabidhi madawati hayo kwa mkuu wa shule hiyo Suleimani Shabani Kipanya na kusema kuwa lengo la kutengeneza madawati hayo limetimia kwa asilimia tisini ambapo walitarajia kukabidhi madawati miamoja kutokana na baadhi ya wazazi kushindwa kukamilisha michango yao kwa wakati.

 kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule hiyo Suleimani  Kipanya ameshukuru wazazi hao kwa kujali maendeleo ya watoto wao katika suala zima la kuchangia miradi ya maendeleo ya shule hiyo hali ambayo itawafanya wanafunzi hao kuongeza kiwango cha kufauru kutokana na mazingira ya shule kuwa mazuri.

Kipanya amesema  kuwa  zaidi ya madarasa mawili ya wanafunzi katika shule hiyo walikuwa wanasoma huku wamekaa chini  zaidi ya miaka miwili  pia kwa kuanza na  mwaka huu 2014 tatizo hilo limekwisha na hakuna mwanafunzi anayesoma huku akiwa amekaa chini.

Amesema  shule hiyo mpaka hivi sasa itakuwa na jumla ya madawati 300 huku ikiwa na jumla ya wanafunzi 1200 pamoja wanafunzi wa  darasa la awali 126, walimu ishirini na saba wakiume wawili,wakike ishirini na tano na  ilianzishwa mwaka 1975.

Aidha kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa mbuyuni Chief Abdalah Sube  ambaye  alishuhudia ukabidhiwaji wa madawati hayo amesema kuwa jambo walilolifanya wazazi hao ni jema huku akiwataka wazazi wengine waige mfano huo kwani kusomesha watoto katika mazingira mazuri ni kuwapatia urithi wa elimu bora.

Sube amesema  baadhi ya wazazi katika shule za msingi
  wamekuwa na tabia ya kuchanganya masuala ya siasa na maendeleo  ambapo suala likipelekwa hivyo linafanya  kushindwa  kukamilisha michango ya madawati kwa ajiri ya watoto wao hivyo kuwafanya wakiendelea kukaa chini pasipo na sababu za msingi.

0 Response to "WAZAZI NA WALEZI WAKABIDHIWA MADAWATI KWA PESA WALIZOKUWA WAMECHANGA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.