Habari za hivi Punde

MKUU WA MKOA WA SHINYANGA AZINDUA BODI YA RUFAA YA MKOA

Mkuu wa mkoa wa shinyanga Ally Nassoro Rufunga juzi amezindua rasmi bodi ya hospitali ya rufaa ya mkoa huku akiwataka wajumbe wa bodi hiyo kufanya kazi kwa ufanisi ili kuboresha mfumo wa uendeshaji wa hospitali ya mkoa wa shinyanga.


Bodi  hiyo itakuwa na  wajumbe 17 pamoja na  mambo mengine inajukumu la kushirikiana na wadau wote wa afya mkoani Shinyanga lengo likiwa ni kuboresha upatikanaji wa huduma hiyo.

Katika uzinduzi wa bodi hiyo, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa mkuu wa mkoa, Rufunga ametoa rai kwa bodi hiyo kufanya vikao kwa mujibu wa sheria pamoja na kusimamia vyanzo vya mapato ya fedha na matumizi ili kuongeza kiwango cha huduma ya afya katika mkoa wa shinyanga.


Awali akiongea katika uzinduzi huo mganga mkuu wa mkoa wa shinyanga  Dkt Ramadhani Kabala amesema bodi hiyo inatokana na mabadiliko endelevu katika sekta ya afya chini ya mkakati wa pili ambao unalengo la kuimarisha uwezo wa hospitali za mkoa na kanda ili ziweze kutoa huduma bora za rufaa.

0 Response to "MKUU WA MKOA WA SHINYANGA AZINDUA BODI YA RUFAA YA MKOA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.