Habari za hivi Punde

IDARA YA UHAMIAJI MKOANI SHINYANGA INAKABILIWA NA CHANGAMOTO MBALIMBALI.


IDARA ya uhamiaji mkoani Shinyanga  inakabiliwa changamoto wa vitendea kazi kwa kukosa  magari ya kutosha ,kutokuwa na sare maalumu zinazoendana na mazingira ambazo zinaweza kuhimili mazingira ya kikazi na hivyo kushindwa kufanya kazi yao ipasavyo ya kudhibiti wahamiaji haramu wanaoingi
 
Hayo yalibainishwa  na mtumishi wa Idara ya uhamiaji mkoani humo Herieti Mayunga wakati akisoma Risala  kwa mgeni Rasmi katika sherehe ya kuuaga mwaka 2013 na kuukalibisha mwaka 2014 iliyofanyika mjini shinyanga na kuhusisha wakuu wa idara ya uhamiaji kutoka mikoa ya Geita,Mwanza, simiyu pamoja na Mara.
 
Herieti alisema licha ya upungufu wa vitendea kazi hivyo , pia idara hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali likiwemo suala la uhaba wa watumishi ambapo idara hiyo kwa mkoa mzima inawatumishi 33, pamoja na kukosa ushirikiano wa kutosha kwa wananchi wa kuwafichua wahamiaji hao haramu
 
Naye Afisa uhamiaji mkoa wa shinyanga AnnaMaria Yondani aliwataja wahamiaji haramu waliokamatwa mkoani humo, na wanaoishi kinyume na sheria kuanzia kipindi cha Januari hadi Desemba mwaka jana ni wahamiaji  162, walioondoka kwa OD 19,  PI 75 , waliofungwa 30, waliochiwa huru na kuambiwa kufuata taratibu za nchi 32 na kesi zinazoendelea 6.
 
Pia alitaja sababu zinazochangia kuongezeka kwa wahamiaji haramu mkoani humo ni kutokana na uwepo wa migodi ya madini ya Dhahabu , Almasi, kilimo cha Pamba, Tumbaku, pamoja na Barabara kuu iendayo Rwanda, Burundi, Uganda, Kongo DRC, hali ambayo husababisha ongezeko la watu wengi hasa katika wilaya ya kahama ambayo imekuwa ikikithili kwa wahamiaji hao.
 
Kwa upande wake mgeni Rasmi mkuu wa mkoa shinyanga Ally Rufunga aliahidi  suala la upungufu wa vitendeakazi atalifikisha katika ngazi ya taifa kwani hilo lipo nje ya uwezo wake huku akiwataka watumishi wa Idara hiyo kufanya kazi kwa kuzingatia misingi ya sheria na taratibu za nchi  pamoja na kujiepusha na vitendo vya rushwa.
 
‘’Idara ya uhamiaji huwa inakabiliwa na rushwa , hasa pale mnapo wakamata wahamiaji haramu kutoka sehemu mbalimbali wakiwemo wa Somali wamekuwa wakiwapa fedha na kuwa achia waendelee na shughuliza zao, hivyo na toa onyo kwenu atakaye bainika kuhusika na vitendo vya rushwa sheria itachukua mkondo wake” alisema Rufunga.
 
Akizungumza katika sherehe hiyo Afisa uhamiaji mkoa wa Mwanza Remegius Pesambili alitoa ushauri kwa Idara ya uhamiaji  licha ya mapungu waliyonayo bali washirikiane na vyombo vya ulinzi na usalama kwa kuhakikisha wanatokomeza au kupunguza wahamiaji haramu mkoani humo.
 
Alisema wahamiaji hao wanapokithiri hapa nchini huweza kusababisha kuwepo kwa matukio ya kigaidi kwani asilimia kubwa ya matukio hayo hutokana na watu kutoka nchi za jirani.
 

0 Response to "IDARA YA UHAMIAJI MKOANI SHINYANGA INAKABILIWA NA CHANGAMOTO MBALIMBALI."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.