Habari za hivi Punde

MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI KUTOKA KWA MAMA KWENDA KWA MTOTO YAPUNGUA NA KUFIKIA ASILIMIA 5.6 MKOANI SHINYANGA



WANANCHI  mkoani  shinyanga  wametakiwa kuondokana na  unyanyapaa kwa watu walioathirika na virusi vya ukimwi  ikiwemo mama wajawazito kuhudhuria  katika kliniki  kwa  kupima afya zao na  kuondoa maambukizi ya  mama kwenda kwa mtoto ambapo kiwango mpaka sasa kimefikia asilimia 5.6.

Hayo  yalisemwa na  mkuu wa wilaya ya Shinyanga Annarose Nyamubi kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga  kwenye uzinduzi wa  kampeni ya utokomezaji  wa maambukizi  virusi vya ukimwi  toka kwa mama  kwenda kwa  mtoto huku akisema kuwa  maambukizi  hayo tangu mwaka 2011 yalikuwa asilimia 26.


Nyamubi alisema kuwa  mkoa umepiga hatua kubwa ya kuweza kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi  kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ,ikiwa suala la unyanyapaa bado ni tatizo kubwa katika jamii hivyo kwa kushirikiana kwa pamoja  maambukizi hayo yanaweza kutokomezwa  na kuondoa unyanyapaa.

“Kweli maambukizi ya virusi vya ukimwi sio tishio la kuweza kumuogopa mtu kwani ni kama magonjwa mengine  kinachotakiwa  jamii kushirikiaana kwa kufuata  wataalamu wa afya wanavyosema  kama mtu anakuwa hajaathirika basi atajilinda na yule ambaye atakuwa amegundulika  atapata ushauri wa kuweza kuishi vizuri kwenye jamii na mwenza wake”alisema Nyamubi.

Alisema kuwa  kwa takwimu za kitaifa   kwa mwaka wa 2010 zilikuwa ni asilimia 5.3 ambapo katika mkoa wa Shinyanga  mpaka sasa unamaambukizi ya asilimia  7.4 kwa takwimu za mwaka wa 2012,ambapo alidai kuwa kwa pamoja kwa kushirikina ugonjwa huo unaweza kutokomezwa  na usiwepo .

 Mganga mkuu wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga  Dkt Ntuli  Kaborogwe  alisema  ushauri uliopo  kwa wananchi kuwa ifikapo mwaka wa 2015 mkoa huu uondokane na maambukizi mapya  ya virusi ikiwa idadi ya maambukizi inaenda ikipungua tofauti na miaka mingine ya 2011 kuwa asilimia na asilimia 26 na kupungua kufikia asilimia 5.6 mwaka 2012.

Kwa upande wake  meneja wa shirika lisilo la kiserikali  linalotoa elimu dhidi ya kujikinga na  virusi vya ukimwi  (Agpahi) kwa mkoa wa Shinyanga  Dkt Gastor Njau alisema kuwa  uzinduzi wa kampeni hii lengo lake ni utokomezaji  wa maambuziki ya  virusi vya ukimwi  kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto katika  hatua muhimu  ya kuondoa  ukimwi kwa watoto.

Hata hivyo Ngwashi Salehe ni mmoja wa shuhuda aliyejieleza katika hadhara iliyohudhuria uzinduzi huo  kuwa ni mwaathirika tangu mwaka 2002  na kuendelea kunywa  ARV kwa  kubahatika kupata mtoto mwaka 2012 akiwa hajapata maambukizi yoyote  kutoka kwa mama ambapo alieleza pia ni kutokana na kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya na kuzingatia  maelekezo.

0 Response to "MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI KUTOKA KWA MAMA KWENDA KWA MTOTO YAPUNGUA NA KUFIKIA ASILIMIA 5.6 MKOANI SHINYANGA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.