Habari za hivi Punde

WAFANYABIASHARA SOKO LA NGUZONANE WALALAMIKIA ONGEZEKO LA USHURU





WAFANYABIASHARA  wa vibanda katika soko la Nguzo nane manispaa ya Shinyanga mkoani hapa wamelalamikia ongezeko la kutozwa ushuru kutoka shilingi 15,000 na kupandishiwa shilingi 30,000 jambo ambalo wamemuomba mkurugenzi wa manispaa hiyo Festo Kang’ombe kuongea nao ili kutatua suala hilo.

Wafanya biashara hao wakizungumza na waandishi wa habari katika soko hilo jana walisema kuwa kilio chao kikubwa ni kumuomba mkurugenzi wa manispaa hiyo waongee nae kwani wamekuwa wakipandishiwa ushuru bila hata kuwashirikisha wao hali ambayo wanadai wananyongwa kulingana na kipato kidogo wanachokipata katika biashara zao.


“Kwa kweli ongezeko hili hatulikubali kwani manispaa hatuielewi ina mpango gani na sisi ukilinganisha na hali ya hewa ya sasa siyo nzuri kipato tunachokipata ni kidogo sana lakini manispaa inatupandishia ushuru tumeamua kwenda kwa mwanasheria wa manispaa lakini majibu yake yamekuwa yakitatanisha”walisema wafanyabiashara hao.

“Kilio chetu sisi wafanyabiashara ni kutaka kuongea na mkurugenzi wa manispaa kwani mwaka 2011 nikiwa kama wakala tulikuwa tunatoa ushuru shilingi 1500 lakini ukapandishwa shiringi 15000 ambapo haileweki mara unatozwa elfu 20 na sasa kuanzia tarehe 1 mwezi wa 3 mwaka huu wanatupandishishia elfu 30 huku wakala anaechukua ushuru haelewi ongezeko hili limeongezwaje”alisema Abdul Kidoda ambaye ni mfanyabiashara katika soko hilo.

Akizungumzia suala hilo mwenyekiti wa wafanyabiashara katika soko hilo Hassan Baruti alisema kilio chao kikubwa ni kupandishiwa ushuru kwani kwa sasa hali ni mbaya ya kibiashara wafanyabiashara hawapati kipato kikubwa wanawatotot wanasomesha hivyo alimuomba mkrugenzi awakubalie aje awasikilize kilio walichonacho.

“Sheria hii inayotarajiwa kuanza tarehe moja mwezi wa tatu itawaumiza sana wafanyabiashara wa soko hili tunasikia diwani wa kata hii ndiye aliyepitisha ongezeko hili lakini hahudhulii hata kwenye vikao vyetu kusikiliza matatizo tuliyonayo katika biashara”alisema Baruti.

Salome Ntalimbo ambaye nae ni mfanyabiashara wa soko hilo alisema wao walikubaliana na shilingi 15000 na wakasaini mkataba na kuanza kulipa sasa mwaka huu wametupandishia ushuru hali ambayo imetufanya tuchanganyikiwe kutokana na ongezeko hilo.

"Tunamuomba tu mkurugenzi akubali tuongee nae ili tuweze kuyamaliza kwani wakati huu tunahali ngumu sana ya kipato ukilinganisha na sisi wenyewe tuna watoto tuna somesha na ushuru wa manispaa unazidi kupanda huku tunatakiwa kulipa mikopo tuliyokopa"alisema Ntalimbo.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa manispaa hiyo Mwanamisiyu Dossi ambaye pia ni afisa ustawi wa jamii alisema kuwa suala hilo watalifuatilia.

0 Response to "WAFANYABIASHARA SOKO LA NGUZONANE WALALAMIKIA ONGEZEKO LA USHURU"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.