Habari za hivi Punde

KUMOMONYOKA KWA MAADILI KUMEFANYA VITENDO VYA RUSHWA KUSHAMIRI NA KUCHAKACHUA MIRADI




 KUMOMONYOKA  kwa maadili kwa baadhi ya watumishi wa
 umma ni moja ya sababu zinazochangia kukithiri kwa vitendo
 vya rushwa na kuchangia kuongezeka uchakachuaji wa miradi ya
 maendeleo, unaofanywa na wakandarasi kwa kushirikiana na
 wataalamu nakuwataka wanaofanya vitendo hivyo kujitathimini
 wenyewe  kuachia ngazi zao kabla ya kuwajibishwa.
 
Hayo yalielezwa jana na kamanda wa taasisi ya kuzuia na kupambana na  rushwa (TAKUKURU )mkoa wa Shinyanga Gasto Mkono, kwenye kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa huo,ambapo alisema viongozi na  mamlaka husika zikiwa zimekaa kimya bila kuchukuwa hatua hali ambayoinatoa picha kuwa watawala hao ni waoga
wakushiriki katika vita dhidi ya rushwa.

 
 Alisema katika kukabiliana mapambano ya tatizo la rushwa
 kuna  changamoto ambazo ni kikwazo ukiwemo mtazamo
potofu wa baadhi ya wanajamii kuwaona wanaojihusisha na
 vitendo vya rushwa na wahujumu uchumi kama mashujaa,ushahidi
 kukosekana,ushirikiano hafifu toka katika baadhi ya taasisi
 hasa zinapokuwa zinachunguzwa pamoja na ukosefu wa fedha
 hususani kwenye uchunguzi na uendeshaji kesi kubwa .

 Ni vema watumishi wa umma wakajitathimini wao wenyewe
 uhalali wao wa kuendelea kuwepo katika nafasi walizonazo
 wakati wanashindwa kupambana na rushwa,hivi sasa mkoa wa
 Shinyanga katika kipindi cha januari hadi Desemba 2013 ni
 kesi 15 zilipatikana kati ya hizo idara ya afya ni
 tisa,elimu tatu na halmashauri tatu zilizolenga
 Tasaf”alisem.

 Akizungumza kwenye kikao hicho waziri wa nchi, ofisi ya rais
 utawala  bora Kapten mstaafu George Mkuchika,alisema
 iwapo kila moja atazingatia maadili ni wazi hata vitendo vya
 rushwa vitapungua tofauti na hali ilivyosasa rushwa
 imekithiri na kuwaathiri zaidi wananchi masikini ambao
 hawana kipato hasa wanapohitaji kupata huduma ya
 matibabu,dhamana,elimu na kufuatilia mafao.
 
 Alisema rushwa ndogo ambayo inawalenga zaidi watumishi wa
 ngazi za chini hasa wakati wa kutoa huduma, inawatesa
 wananchi maeneo mengi na kufikia hatua ya kuichukia serikali
 iliyokomadarakani kwa kushindwa kupata huduma,na kutolea
 mfano wa rushwa kubwa ambayo inaleta athari kubwa kiuchumi
 kutokana na uroho ,tama na ubinafsi wa kujilimbikizia mali
kwa haraka.
 
 Waziri mkuchika alisema utawala bora ukiwepo matatizo hayo
 hayatakuwepo,ambapo uliutaka mkoa wa Shinyanga kuachana na
imani potofu za kishirikina zakuuwa vikongwe na albino hali
 hiyo inatokana na ukosefu wa elimu na hofu ya mungu,na
 kwamba mtu anapozeeka anatakiwa kupongezwa na kupewa zawadi
na siyo kumkata mapanga kwa kumtuhumu kuwa mchawi.
 
 Awali mkuu wa mkoa huo Ally Rufunga akimkaribisha
 waziri,alitoa wito kwa watumishi wa umma na wananchi kwa
 ujumla kujiunga na bima ya maisha ambayo itawasaidia
baadaye,na kusisitiza umuhimu wa kupanda miti ili kuhifadhi
 vyanzo vya maji visitoweke na wananchi kukosa huduma ya
 maji. Shinyanga

0 Response to "KUMOMONYOKA KWA MAADILI KUMEFANYA VITENDO VYA RUSHWA KUSHAMIRI NA KUCHAKACHUA MIRADI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.