Habari za hivi Punde

VIONGOZI WA VIJIJI WILAYANI KISHAPU WAAGIZWA KUSIMAMAIA MAZINGIRA IKIWEMO UFUGAJI WA NYUKI KATIKA MISITU.



VIONGOZI  wa vijiji wote wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga wameagizwa kuhakikisha wanasimamia mazingira ipasavyo, na wahakikishe miti  haikatwi kiholela ili kuimarisha ufugaji wa nyuki katika misitu hiyo. 

Agizo hilo limetolewa jana na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Willison Nkhambaku wakati wa uzinduzi wa mizinga ya nyuki uliofanyika katika kijiji cha Nyasamba kata ya Bubiki wilayani humo ambapo alisema atakaebainika anakata ovyo achukuliwe hatua kali za kisheria.


“Nawaomba sana viongozi wa vijiji simamieni miti isikatwe katwe ovyo atakayeonekana anakata miti tutamchukulia hatua kali za kisheria hivyo tuhakikishe tunalinda miti yetu ili tuweze kupata nyingi na kuondokana na balaa la njaa”alisema Nkhambaku.

Alisema kiongozi ambaye hata simamia ipasavyo atachukuliwa hatua kali na kama atashindwa achukue jukumu la kujiuzulu kuanzia sasa na kuwataka wasimamie mipaka iliyopo maeneo ya nyuki yaheshimiwe.

“Sisi viongozi tukisimamia vizuri itasaidia kuinua kipato kwa kupitia ufugaji wa nyuki ambayo inafaida nyingi unaweza ukatengeneza dawa ya kuondoa fangazi, kupunguza mvi kwa wazee, kutengeneza ngozo iliyokunjamana, kutengeneza mshumaa ambao utauwasha na kuweza kukimbiza mbu na faida zingine mbalimbali”alisema Mkuu huyo.

Akisoma taarifa ya wanakikundi cha ufugaji nyuki kwa wazee chenye jina la Upendo- kilichopo kijiji cha Nyasamba Willison Malimu ambaye ni katibu wa kikundi hicho alisema mradi huo wa ufugaji wa nyuki ulianza rasmi tarehe 9/4/2011.

Alisema mradi huo ulianza ukiwa na wanachama 15 kwa manufaa ya kuinua hali ya maisha ya wanakikundi pindi mradi utakapo  anza kutoa mazao ya nyuki (Asili na nta).

Alisema katika mradi huo kuna changamoto nyingi ambazo ni wananchi kuingia na kukata miti katika misitu, wananchi kuingia eneo la msitu na kulima, mifugo kuingia katika msitu kulisha humo ikiwa ni pamoja na msitu kuharibiwa na kusababisha kutokueleweka mwisho wake.

Katibu wa kikundi hicho alisema kikundi hicho kiliomba fedha toka mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) na kukubaliwa ambapo walipewa  jumla ya Tshs 11,855,301.50/= ambazo walitumia kwa kupatiwa mafunzo kwa ajili ya uendeshaji wa mradi.

Alisema kupitia fedha hizo pia walipata mafunzo ya ufugaji bora wa nyuki yaliyoendeshwa na idara ya nyuki wilayani hapo, walinunua zana za kufugia nyuki jumla ya mizinga 50, ambapo mizinga ambayo imeanza kutumiwa na nyuki ni saba.

0 Response to "VIONGOZI WA VIJIJI WILAYANI KISHAPU WAAGIZWA KUSIMAMAIA MAZINGIRA IKIWEMO UFUGAJI WA NYUKI KATIKA MISITU."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.