Habari za hivi Punde

CHANGAMOTO KWA WATOTO WENYE VVU NA WENYE KUISHI MAZINGIRA HATARISHI

CHANGAMOTO  kubwa inayowakabili watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi  pamoja na wale wenye kuishi na maambukizi ya virusi vya  ukimwi ni  kwa ukosefu wa mahitaji muhimu wanaopaswa kuyapata kama watoto wengine , lishe duni , pia  walezi au wazazi kutokuwa na kipato huku wengine wakiwatelekeza kwa makusudi.

Hayo yalisemwa na mwalimu  Johari  Salum wa kituo cha kulelea watoto  hao cha (ECD) chini ya ufadhili wa shirika la Lara Foundation International  kilichopo kata ya Ndala manispaa ya Shinyanga  chenye watoto 45, wakati wa mfanyabiashara Oscar Kaijage  alipotembelea  kituoni hapo akiwa ameambatana na mke wake  kwaajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali  yakiwemo madaftari na kalamu.

Mwalimu Salum alisema kuwa changamoto kubwa inayowakabili watoto hao ni kutokuwa na lishe nzuri,walio wengi wanaishi na walezi wao ambapo wazazi wengine walikwisha fariki kwa maambukizi  ya virusi vya ukimwi huku walio bado hai wamekwisha watelekeza  kutokana na kipato duni  kwenda kutafuta maisha.

“Kituo hicho tumechukua  watoto wenye hali mbalimbali katika maisha yao ili waweze kupata elimu ya awali,lakini  walengwa wanaotakiwa kuwepo kwenye kituo hicho ni watoto wenye kuishi na maambukizi ya virusi vya ukimwi na mazingira hatarishi kwani wanaoishi na virusi pekee katika tathimini iliyofanyika maisha yao waliowengi yenye uafadhali kuliko  hata  ambaye hana maambukizi hayo hivyo tunaangalia kipato cha familia kikoje”alisema mwalimu Salum.

Naye kaijage alisema kuwa aliamua kutoa msaada huo wa vitu mbalimbali  kwa kuona yuko sahihi  kwa pamoja kuwa na watoto hao kwani hata yeye ni yatima  aliyefiwa na mama yake mzazi kutokana na  maradhi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi huku akieleza kuwa   uhalisia watoto hukosa malezi yaliyobora  na vitu  wanavyovihitaji ni adimu kwao na kuishia kuvitamani.

“Msaada huu ni kama kumbukumbu ya  mama yangu mzazi kwani nilihitaji zaidi awepo lakini hakuna budi  ya kukumbuka  kwa kutoa msaada kwa watoto hao ambao baadhi yao ni yatima,weninge wanaoishi katika mazingira hatarishi kutokana na walezi au wazazi kuwa na kipato duni ambapo vitu vingi hutamani na kuwa nadra kwao kuvipata”alisema Kaijage.

Kwa upande wake  mwenyekiti wa mtaa wa  Mlepa  John   Buhembo alisema kuwa kituo hicho kimekuwa na utaratibu wa kuwapata watoto hao kama ilivyolengwa ,aliitaka  jamii ishirikiane  ili iweze kuwasaidia watoto hao  kufanikisha maendeleo na kuacha kuingiza  mambo ya siasa kwa wazazi au walimu ,kama yataingia ndani ya kituo hicho hakika hakita dumu .

0 Response to "CHANGAMOTO KWA WATOTO WENYE VVU NA WENYE KUISHI MAZINGIRA HATARISHI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.