Habari za hivi Punde

WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO ZAIDI HUPATA UPUNGUFU WA DAMU NA MALARIA

CHANGAMOTO kubwa inayowakumba  watoto waliochini ya umri wa miaka mitano  kiafya ni upungufu wa damu na ugonjwa wa malaria  hali ambayo inapekekea kuleta msongamano wa wagonjwa katika kituo cha afya kilichopo kata ya Iselamagazi tarafa ya Nindo wilayani Shinyanga.

Akiongea na waandishi wa habari waliokuwa wametembelea  katika kituo hicho mganga mkuu wa  Dkt Heleni Kaunda  aliwaeleza kuwa msongamano wa wagonjwa pia unaletwa kwa kuhudumia  wagonjwa ambao wanahitaji matibabu zaidi kutoka zahanati sita zinazozunguka kata hiyo.

Dkt  Kaunda alibainisha kuwa watoto waliochini ya  umri wa miaka mitano  zaidi ndio wamekuwa wakipata ugonjwa wa malaria ya homa kali pamoja na upungufu wa damu hali ambayo inaleta msongamano  ikiwemo kuhudumia kwa masaa 24.



“Msongamano wa wagonjwa upo,wengi  wamekuwa wakipelekwa rufaa  kwa malaria kali na upungufu wa damu ikiwa zaidi watoto  kwa siku  wawili mpaka wanne, pamoja na akina mama wanaoshindwa kujifungua “alisema Dkt Heleni.

Pia Shija Ramadhani mkazi wa kijiji cha Iselamagazi alionekana kuhudhuria katika hospitali ya mkoa huku akiwa amembeba mtoto wake mgongoni  baada ya kuulizwa na mwandishi alidai kuwa mtoto huyo alilazwa katika kituo cha afya  lakini hali ilionekana kuwa mbaya kutokana na kutopatiwa dawa tangu alazwe.

Naye afisa mtendaji wa kata  Paul Kulwa alisema kuwa kata ya Iselamagazi  inazahanati mbili ambazo zipo katika vijiji vya Mwamakaranga na Homango  ambapo inahudumia zaidi ya vijiji sita  pamoja na kata ya Lyabusalu mpya yenye vijiji  saba  ikiwemo vijiji vya jirani ya wilaya ya Kishapu na mkoa wa Mwanza.

Hata hivyo alisema kuwa  kata hiyo inaidadi ya  watu zaidi ya 20,000  vituo vya kutolea huduma  ya afya vichache  na upatikanaji wa dawa unakuwa wa shida kwani huja chache  ambazo hazitoshelezi  idadi ya watu waliopo na wanaotoka nje ya kata hiyo.

Aidha baadhi ya  wananchi wa kijiji cha Mwamakaranga  Rafael Paul na shija Masalu walisema kuwa  upatikanaji wa huduma umekuwa shida ziku zote kutokana na msongamano wa wagonjwa katika zahanati na kituo cha afya ikiwemo kukosa madawa hivyo hulazimika kwenda kununua dawa.

Changamoto hiyo imetokana na zahanati pamoja na vituo vya afya hasa vijijini kutokuwa nadawa hata kama zikiletwa hazikidhi  matakwa ya  idadi ya  watu  waliopo kwenye eneo husika ,ambapo jamii huamua kwenda kununua kwenye maduka binafsi huku zingine zikiwa feki.

Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dtk Fredrick Mlekwa alisema kuwa kweli wagonjwa wanaotoka nje walio wengi ni kutoka maeneo ya vijijini,wakifika hapa wanakuwa na hali mbaya kiafya hiyo inatokana na uelewa mdogo wa wananchi hao au huduma zinazotolewa katika vituo vya afya na zahanati pamoja na za watu binafis kuwa na kiwango kisichokidhi kiafya kwa kujali maslahi yao.

Naye mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga alisema kuwa  mkoa huu umetenga jumla ya shilingi  billion 3.5 kwaajili ya  kukabiliana na changamoto mbalimbali za kupata afya bora katika jamii ambapo  mpaka sasa ni asilimia 70 ya vituo vya afya na  zahanati ni asilimia 60 huku halmashauri mbili zikiwa na hosptal.

0 Response to "WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO ZAIDI HUPATA UPUNGUFU WA DAMU NA MALARIA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.