Habari za hivi Punde

PSPF YATOA ELIMU KWA WAJASILIAMALI SOKO KUU MANISPAA YA SHINYANGA.




WAJASILIAMALI   wenye kipato kidogo manispaa ya Shinyanga   wametakiwa kujiunga na  mfuko  wa Pensheni kwa watumishi wa Umma ( PSPF) mara baada ya  kutolewa   elimu   ikiwa imebainika  kuwa asilimia kubwa bado hawajajiunga na  mfuko huo kwa dhana iliyojengeka  kuwa ni kwaajili ya watumishi pekee.

Inatakiwa wajasiliamali waone  umuhimu wa kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii hapa nchini na kuweza kunufaika nayo  kwa kutunza fedha ambazo zitawasaidia katika maisha ya sasa nayabaadae.

Akitoa elimu hiyo kwa wajasiliamali wa soko kuu la mjini Shinyanga  mjumbe wa Bodi wa mfuko huo kutoka Jijini Dar es salaam  Clement  Mswanyama alisema asilimia kubwa ya wajasiliamali hapa nchini hawajajiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii na kuwafanya  kukosa fedha za kuwasaidia katika maisha hasa pale wanapopatwa na matatizo.

 “ Watu wanaofanya shughuli zenye kipato kidogo  asilimia kubwa wamekuwa wakisahaurika kupewa fursa ya kujiunga na mifuko hiyo ya hifadhi ya jamii na kuwathamini watumishi ambao wameajiriwa hali ambayo huwajengea watu hao mazingira ya kuwa na maisha magumu”alisema .


Alisema  mtu  anapojiunga na mfuko wa hifadhi ya jamii itamsaidia kujiwekea hazina ya fedha ambazo zitamsaidia katika maisha yake hasa pale anapopatwa na matatizo ya kifamilia ikiwa ni pamoja na kupata mafao yake ya uzeeni na hivyo kumfanya kuendelea kuwa na maisha.

Alibainisha kuwa shirika hili la  PSPF lilikuwa linahudumia  watumishi wa serikali peke yao lakini kutokana na serikali kuona idadi kubwa ya wafanyabishara wa kujitegemea kusahaulika kupewa fursa ya kujiunga na mifuko hiyo ambapo imeweza kupanua wigo na kuwapa nafasi wajasiliamali kuchangia fedha kidogo kidogo kwa kila mwezi katika mfuko huu ilikuboresha maisha yao.

Naye meneja wa Shirika hilo mkoani Shinyanga  Elick Chanimbaga  alisema wameamua kutoa elimu hiyo kwa wajasiliamali wote mkoani  hapa  kwa kushirikisha wafanyabishara wa masoko, mama Lishe,waendesha bodaboda, wafanyakazi wa viwandani na lengo kubwa likiwa ni kuwajengea msingi mzuri wa maisha kutokana na utunzaji wa fedha katika mifuko ya hifadhi ya jamii.

Kwa upande wao  baadhi ya wajasiliamali wa soko hilo  James  Jilinde  na Hawa  Ngoshaji kwa nyakati tofauti walishukuru elimu iliyotolewa huku  wakidai kuwa walikuwa hawajui faida ya kujiunga na mifuko hiyo  na kufikiri walengwa ni watumishi wa serikali pekee.

0 Response to "PSPF YATOA ELIMU KWA WAJASILIAMALI SOKO KUU MANISPAA YA SHINYANGA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.