Habari za hivi Punde

WANAFUNZI 47 WASHINDWA KURIPOTI KUANZA KIDATO CHA KWANZA.



WANAFUNZI  47  waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza mwaka 2013/14  katika shule za sekondari  zilizopo manispaa ya Shinyanga hawajaripoti shule  na kutojulikana walipo.

Hayo yalisemwa na ofisa elimu wa shule ya sekondari  manispaa ya Shinyanga  Daud Mkumbwa  kwenye kikao  kilichojumuisha viongozi wa sungusungu kutoka wilaya za manispaa,shinyanga na Kishapu kwaajili ya kujadili ajenda  ya utoro mashuleni.

Mkubwa alisema kuwa  kumekuwepo na wimbi la utoro mashuleni ikiwemo wanafunzi wa kike kupata mimba, kutohuduria masomo mara kwa mara  ikiwa  wanafunzi wakiume ni 21 na wakike 26 hawajaripoti  shule mpaka sasa,ambapo aliwataka viongozi hao kushirikiana ili kuweza kuondoa changamoto hiyo.

“Manispaa ya Shinyanga inajumla ya shule 17 za sekondari idadi ya wanafunzi 2285, ikiwa  mpaka sasa kunawanafunzi  2035 walioripoti wakiume ni 1013 na wakike ni 1022 ,ambapo  wanafunzi 73 walibadilishiwa shule  kwenda sekondari za binafsi”alisema Mkubwa.

Alisema kumekuwepo na tabia ya baadhi ya wanafunzi  kukaa shuleni kwa muda mfupi na baadaye kurudi nyumbani , ndoa za utotoni kuendelea kutokea huku wengine kupewa mimba hivyo jeshi la sungusungu  wanatakiwa kufuatilia  mienendo ya wanafunzi ili kubaini maendeleo yao kimasomo.

Naye katibu wa  sungusungu tawi la Ikonongo  Selemani  Kanoni  alisema kuwa  watoto wa shule  wanaopata mimba  wamekuwa wakiwataja madreva wenye magari makubwa  huku wazazi nao wakifanya siri jambao ambalo linakuwa ni vigumu kubaini waliowapatia mimba.

“Sisi sungusungu tutaendeleo  kujitahidi kuwasaka na kuwakamata ila wazazi nao watoe ushirikinao,  tatizo lililopo wanafunzi wengi wanaopewa mimba huwataja madreva wenye magari makubwa hivyo inashindikana kuwapata kiurahisi  ili wafikishwe katika vyombo vya sheria huku  baadhi  ya wazazi wakimalizana na aliyempa mimba kinyemela”alisema.

Hata hivyo mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga alisema kuwa  wanafunzi ambao  wameshindwa kuripoti shule  kwa sababu zisizo za msingi wazazi wao wahojiwe na kuchukuliwa hatua ya kufikishwa kwenye vyombo vya sheria kwa kupitia viongozi wa vitongoji,vijiji na kata .



0 Response to "WANAFUNZI 47 WASHINDWA KURIPOTI KUANZA KIDATO CHA KWANZA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.