Habari za hivi Punde

JELA MIAKA 30 KWA KUKUTWA NA PEMBE ZA NDOVU MBILI



MAHAKAMA  ya wialya ya Bariadi Mkoani Simiyu imemuhukumu Mkazi wa mmoja liyejulikana kwa jina la Maganzo Zelamoshi mkazi wa kijiji cha Zangho kata ya Mwabali wilayani humo, kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na nyara za serikali bila ya kibali.

 Akimsomea shtaka linalomkabili mtuhumiwa kabla ya hukumu hiyo Mwendesha mashtaka wa TANAPA Eliasi Benjamini, alisema kuwa mnamo tarehe 21 octoba 2013 mtuhumiwa alikutwa akiwa na pembe 2 za ndovu.


 Alisema mtuhumiwa huyo alikutwa na pembe hizo mali ya serikali bila ya kibali maalumu, ambapo alikamatwa na kufikisha mahakani, huku mali hiyo ikiwa yenye  dhamani ya shilingi Milioni 760.

 Akitoa hukumu hakimu mkazi wa mahakama hiyo Robert Oguda  alisema mahakama imemtia hatiani mtuhumiwa kutokana na ushaidi uliotolewa na upande wa mashtaka na kuamuli kwenda jela kifungo cha miaka 30 pamoja na kulipa faini ya shilingi Milioni 17.

0 Response to " JELA MIAKA 30 KWA KUKUTWA NA PEMBE ZA NDOVU MBILI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.