Habari za hivi Punde

ALBINO AUWAWA KIKATILI WILAYANI BARIADI

Bariadi. Matukio ya kuuawa kwa watu wenye ulemavu wa Ngozi (Albino) yamezuka upya mkoani Simyu, ambapo mwanamke mmoja Mughu Lugata (40) mwenye ulemavu wa ngozi (Albino) ameuawa kinyama kwa kukatwa katwa mapanga na watu wasiojulikana pamoja na kutoweka na baadhi ya viungo vyake.
 
Tukio hilo lililotokea katika kitongoji cha chalala kijiji cha Gasuma kata ya Nkololo wilayani Bariadi Mkoani hapa, marehemu alikatwa mguu wake wa kushoto sehemu ya goti, vidole 2 mkono wa kushoto pamoja ukucha wa kidole gumba , ambapo wahusika walitoweka na viungo hivyo.
 
Akitoa taarifa mbele za waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa polisi mkoani hapa Charles Mkumbo alisema kuwa tukio hilo limetokea  jana majira ya saa 12 usiku hadi saa moja hasubuhi,wakati marehemu akiwa nyumbani kwake.
 
“marehemu aliuawa na kiungo chake cha mguu wa kushoto kuchukuliwa kwa kukatwa sehemu ya goti, vidole 2 vya mkono wa kushoto ambavyo ni kidole cha 3 na 4,kukatwa na kuchuliwa na ukucha wa kidole gumba cha mkono wa kushoto na viungo vyote hivyo vilitoweka na wahusika wa mauaji hayo” Alisema Mkumbo.
 
Alisema kuwa akiwa amelala nyumbani kwake peke yake mwasnanmke huyo alivamiwa na watu wasiojulikana na kuanza kumkatakata mapanga na kuchukua baadhi ya viungo vyake vya mwili na kutokomea navyo kusiko julikana .
 
Aliongeza kuwa katika upelelezi wa awali wa jeshi hilo linawashikiria watu wawili ambao ni waganga wa kinyeji Gudawa Yalema (52) msukuma na mkulima wa kijiji hicho.
 
Alimtaja mtuhumiwa mwingine kuwa ni Shiwa Masalu (Uselengi) naye mkazi wa kijiji hicho ambaye alikuwa pamoja na mtuhumiwa wa kwanza wakiwa na vifaa vya kupigia ramli, huku akieleza chanzo cha tukio hilo ni imani za kishirikina.
 
Mkubo amewataka wananchi wenye taarifa juu ya wahusika wa tukio hilo kutoa taarifa hizo kwa jeshi hilo, ikiwa pamoja na kuwataka kutodanganyika kuwa utajiri unakuja kwa imani za kishirikina, bali unaletwa kwa kufanya kazi kwa bidii.
 
Alisema kuna baadhi ya waganga wanawadanganya wateja wao kuwa viungo vya mlemavu wa ngozi vinaleta utajiri hali ambayo inawanafanya baadhi ya watu kuamini na kuendeleza mauaji ya Albino
 
                                          

0 Response to "ALBINO AUWAWA KIKATILI WILAYANI BARIADI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.