Habari za hivi Punde

NJIA YA KUTUMIA SHANGA IMEELEZWA NI BORA ,UZAZI WA MPANGO UNATAKIWA KATIKA JAMII.


Shanga iliyoshikwa mkononi na  mtoa huduma ya afya ya uzazi ambayo imebuniwa na wizara ya afya  kwa lengo la kuwasaidia wanafamilia kupanga uzazi kwa kutumia njia hiyo ambayo imeonekana ni rahisi ,ikiwa njia zote mtu anauhuru wa kuchagua.hivyo jamii imetakiwa kuondoa dhana potofu dhidi ya utumiaji wa njia zilizopo kuwa zina madhara huku wakiziacha na kutumia njia ambazo sio salama.



Hili ni moja wapo la banda lililo kuwa likitoa huduma ya uzazi wa mpango katika  uwanja wa shy-com.
  
 
Wa kwanza kushoto ni Mkuu  wa mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga akiwa na mganga mkuu wa mkoa  Ntuli Kapologwe pamoja na mkuu wa wilaya  ya Shinyanga bi Annarose  Nyamubi wakati wakijiandaa kwenda kukagua mabanda ya watoa huduma za afya ikiwemo uzazi wa mpango ambapo mkuu wa mkoa alizindua  mpango huo huku akiwataka wananchi mkoani humo kutumia njia ya uzazi wa mpango ili kuweza kuleta uiano bora katika malezi ya watoto na kupata mafanikio.


0 Response to "NJIA YA KUTUMIA SHANGA IMEELEZWA NI BORA ,UZAZI WA MPANGO UNATAKIWA KATIKA JAMII."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.