MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KISHAPU MKOANI SHINYANGA JUSTINE SHEKA AKIAHIRISHA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI.
MADIWANI wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu mkoani
Shinyanga wameitaka wizara ya
kilimo,chakula na ushirika
kuhakikisha wanawalipa fidia wakulima wa zao la pamba kwani hivi sasa
wanateseka kwa kukosa fedha na chakula
huku wakishindwa kuendesha maisha
yao, ikiwa zaidi walikuwa wakitegemea
zao hilo kujinyanyua kimapato ndani ya familia.
Sio kwa wakulima pekee hata halmashauri zitapata hasara ikiwa
tayari vibali vimekwisha tolewa kutoka bodi ya pamba
kwa wafanyabishara wa zao la pamba huku wengine wakidaiwa kwenye msimu
uliopita kwa makubaliano
yalivyokuwa mpaka wakiuza ndipo
halmashauri inakata pesa , leo hii zimesitishwa kuchukua ushuru kuna wasiwasi kutorejesha fedha hizo wafanyabishara kwenye halmashauri.
Hayo waliyasema kwenye kikao cha baraza la madiwani liliofanyika katika ukumbi wa halmashauri
hiyo ambapo walimtaka mkurugenzi Jane
Mwitagurwa kuandika barua
kwenda kwa waziri mwenye dhamana kuhakikisha fedha hizo zinalipwa ikiwa
tathimini kwa wakulima tayari huku
uthibitisho wa mbegu zilizotolewa na mkuu wa wilaya pamoja na mkuu wa mkoa upo
mbegu hazikuota.
Diwani wa kata ya Sekebugoro
Ferdnand Mpogomy alisema
kuwa vibali vya ushuru wa pamba vimetolewa na bodi kwa
wafanyabishara ikiwa wengine ni wadaiwa wamepewa vibali hivyo sasa hoja iliyopo
halmashauri imezuwiwa kudai ushuru,
fedha zinazodai wafanyabishara
hao itakuwaje? Waliitaka bodi ya pamba
kujibu namna ya upatikanaji wake ili ziweze kurejeshwa halmashauri.
“Sasa pamba imekosa thamani ni bora wakulima walime mazao
mengine na kuachana na zao hilo, hakika nawaeleza mwakani watalima wachache
mwaka unaofuata hakuna atakaye lima kwani wakulima wameteseka vyakutosha walikuwa wanalitegemea kujinyanyua kimapato ndani
ya familia sasa imekuwa kilio hakuna msaada kinachotakiwa wizara ituhakikishie
ni lini wakulima watalipwa fidia ya
gharama walizotumia?”alisema diwani
Mpogomy.
Diwani kutoka kata ya Mondo John Ndama alisema kuwa katika vikao walivyokaa walidai kuwa
fedha hizo zitalipwa ikiwemo
wakulima kwani wameathirika tangu mwaka
jana mwezi Novemba na tahimini
imeshafanyika walipwe haraka, pia diwani wa kata ya Songwa Mohamed Shabani alisema kuwa maongezi na bodi ya pamba hawataki kwani ndiye aliyesababisha hali kuwa mbaya kwa wakulima kutangaza mbegu
zisizoota ikiwemo madawa feki.
“Mimi kwenye vijiji vya kata yangu wapo watu wa bodi ya
pamba ambao wamekuja kusimamia
,hakuna faida ya kuwepo kwani wameleta uongo kwenye matumizi ya mbegu
zisizo na manyoya , pia inashangazwa wizara kuendelea kuwakumbatia huku ikiwapa jukumu la ukusanyaji ushuru kama
walishindwa kuleta mbegu bora na madawa sasa kwenye ukusanyaji ushuru ndio wataweza au ndio wataiingizia
hasara serikali”alisema diwani wa kata ya Songwa Mohamedi.
Naye mwenyekiti wa halmashauri hiyo Justine Sheka
alisema kuwa wanaiomba serikali
kupitia bodi ya pamba kuhakikisha wanawajali wakulima kwani madiwani wanauwezo wa kuwahamasisha wakulima wa zao la pamba
kuacha kulilima kabisa na kufuata mazao
mengine kutokana na hasara waliyoipata
mbegu kutoota.
“ Tatizo la
mbegu kutoota lilikuwa ni kubwa katika
halmashauri hii wakulima zaidi ya 13OO mashamba yao hayakuota na hivyo
kupata hasara ya zaidi ya billion 1.6.
hiyo yote imetokana na wanasiasa
kudharauliwa na kupuuzwa lakini wangefutilia
tangu mwanzo hasara hii ingekuwa kidogo au isingekuwepo”alisema Sheka.
Kwa upande wake mkaguzi kutoka bodi ya pamba wilaya ya
Kishapu Thomas Tiluhongelwo
alisema kuwa halmashauri
zinahusishwa kupitia kwenye vijiji kufanya tathimini,kuhusu
madawa ya kuua wadudu bod haihusiki, ila
kuhusiana na mbegu mwaka huu watajitahidi
ziwe na ubora pia kabla ya kufikia msimu wa kilimo kuanza wizara imesema itahakikisha wakulima wote waliopata hasara wawe wamelipwa.
|
0 Response to "MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA KISHAPU WAMEIOMBA SERIKALI KUWALIPA FIDIA HARAKA WAKULIMA WA ZAO LA PAMBA WALIOPATA HASARA."
Post a Comment