NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI Philipo Mulugo.
BAADHI ya Walimu wa Shule za Msingi
katika wilaya ya Maswa mkoa wa Simiyu wamepinga mchango wa mbio za Mwenge wa
Uhuru kwa madai kuwa mchango huo ni miongoni mwa michango ya hiari na siyo ya
kulazimishwa wala kutishwa kwa wale ambao hawatachanga mchango huo huku wakidai
mshahara wanaoupata ni kidogo.
Wakiongea na waandishi wa
habari walimu hao walisema kuwa Waratibu
wa Elimu Kata na Walimu Wakuu wanawalazimisha kuchanga mchango huo ambao
wanadai kuwa hawaoni faida yake.
Huku wakikosoa mbio za mwenge wa Uhuru na kutaka ufutwe kwa maelezo kuwa
hauna tija kwa sasa, ambapo baadhi yao wakibainisha kuwa hawako tiyari kutoa
michango huyo kutokana na mishahara yao kuwa kidogo.
“siko tiyari mimi kutoa mchango wangu..kwanza mshahara wangu ni mdogo..hapa
nilipo nina ndugu na wazazi wangu wananitegemea kwa huo mshahara..leo hii
unataka nichangie kitu ambachio sioni faida yake..badala yake kina kula hela
zetu…kwanza wanilipea madeni yangu..ndipo nitatoa michango” Alisema mmoja wa
walimu hao.
Walisema kuwa kama Serikali
inaona thamani ya pesa ya Mwalimu basi ingemwongezea mshahara unaokidhi
mahitaji yake sio kama ilivyo sasa ambapo kiwango wanacholipwa ni mateso na
ambacho wanalazimishwa kuchangia katika mwenge huo.
Wakionyesha
barua ya mchango huo iliyotoka katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri
ya wilaya ya Maswa kupitia Idara ya Elimu iliwaandikia barua Waratibu Elimu
Kata yenye KUMB Na MDC/ADM.10/VO1 1V.105 ya Julai 11 mwaka huu
ikiagiza kuchangia Mbio za Mwenge huku ikiwa imeanisha viwango .
Viwango hivyo kwa mujibu wa barua hiyo iliyosainiwa na Ofisa Elimu Msingi
wilaya ya Maswa,Bujimu Mabeyo inaonyesha kuwa kila mmoja na fedha zao kwenye
mabano Wakuu wa Idara( shilingi 10,000/=),Waratibu Elimu Kata (sh
5000/=),Shule (sh 10,000/=),Mwalimu (sh 2000/=) na CWT
(sh 150,000/=) pia ikasisitiza Waratibu Elimu Kata wapeleke michango
hiyo Julai 31 mwaka huu.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Maswa,Trasias Kagenzi akizungumzia suala
hilo alisema kuwa mchango huo ni moja ya maafikiano yaliyofikiwa katika kikao
ambacho hata Chama Cha Walimu(CWT) waliridhia huku akisisitiza ni wa hiari na
wala hakuna haja ya kushurutishana kwa kuzingatia kuwa imekuwepo kila mwaka .
|
0 Response to "BAADHI YA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI HALMASHAURI YA MASWA WAGOMA KUCHANGIA FEDHA KWAAJILI YA MBIO MWENGE WA UHURU"
Post a Comment