Habari za hivi Punde

WENYEVITI NA VITONGOJI WILAYA YA BARIADI MKOANI SIMIYU WAMEKITAKA CHAMA CHA MAPINDUZI KUMWAJIBISHA DIWANI AMBAYE CHANZO CHA MGOGORO



MWENYEKITI  WA CHAMA CHA MAPINDUZI  (CCM) MKOANI SIMIYU  TITUS  KAMANI.


WENYEVITI  wa Vitongoji katika kata ya Marambo Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu wamekitaka chama cha mapinduzi (CCM) pamoja na serikali kumwajibisha Diwani wa kata hiyo Clementi Matogoro (CCM) kwa madai ya kutumia ubabe katika kuendesha shughuli za kata hiyo.

Mbali na hilo wenyeviti hao wametangaza mgomo wa kutokufanya kazi yeyote ya maendeleo ndani ya kata hiyo, ikiwa pamoja na kutokushiriki katika vikao vya maendeleo vya kata (WDCs), ambapo katika kikao cha maendeleo cha kata kilichofanyika juzi wenyeviti hao walisusia kikao hicho.

Wakiongea na waandishi wa habari katika ofisi za chama cha waandishi wa habari mkoani hapa mara baada ya kususia kikao hicho, walisema kuwa hawako tiyari kufanya kazi na diwani huyo kutokana na kuwatukana pamoja na kuendesha kata kwa ubabe.

Walisema kuwa mbali na ubabe pamoja na kutukanmwa walimtuhumu diwani huyo kuwa chanzo cha wafanyakazi wa serikali ndani ya kata hiyo kufukuzwa kazi, na kuamishwa pindi wanapopinga maamuzi yake.

Walibainisha kuwa Matogoro amekuwa akiongea uongo kwa wakuu wa idara katika halmashauri ya mji ili wafanyakazi hao wafukuzwe kazi au kuamishwa ndani ya kata yake, ambapo waliodai alisababisha mtendaji wa kata pamoja na mwalimu mkuu shule ya msingi Bariadi kuamishwa na kushushwa cheo.

“Tulikaa kikao cha maendeleo ya kata tarehe 16/04/2014..tukakubalina kuuza miti kwa wananchi wetu ambayo ilkuwa imekauka katika pori la marambo..tulipomaliza kikao sisi tulienda kuuza miti hiyo..cha kushangaza..diwani alitugeuka na kuwakamata wananchi wote ambao tulikuwa tumewauzia miti hiyo” Alisema John Masunga Mmoja wa wenyeviti hao.

Walisema kuwa mbali na wananchi hao kukamatwa na kupelekwa kituo cha polisi wilaya diwani huyo aliwatuhumu viongozi hao kuwa ni wezi kwa kuuza miti hiyo kwa maslai yao binafsi jambo walilosema kuwa uongo.

Alipotafutwa na waandishi wa habari kwa njia ya  simu yake ya kiganjani  diwani huyo alikataa kuongelea jambo hilo .






0 Response to " WENYEVITI NA VITONGOJI WILAYA YA BARIADI MKOANI SIMIYU WAMEKITAKA CHAMA CHA MAPINDUZI KUMWAJIBISHA DIWANI AMBAYE CHANZO CHA MGOGORO "

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.