Habari za hivi Punde

UZAZI WA MPANGO MKOANI SHINYANGA WANAOTUMIA NI ASILIMIA 12.5 BADO KUNA CHANGAMOTO KUBWA

WADAU WA AFYA WAKIHAMASISHA  KUFUATA UZAZI WA MPANGO MKOANI SHINYANGA.
BAADHI ya  wazazi  na walezi mkoani Shinyanga wamekuwa  wakiwafanyia unyasaji wa kijinsia    watoto wa kike kwa kuwaoza mapema kabla ya umri wao na viungo kutokukomaa vizuri  kwa lengo la kutaka utajiri wa haraka hali ambayo imeonyesha kuongezeka kwa mimba za utotoni na kufikia asilimia 59 ambapo imeonekana pia  kushindwa  kutumia njia ya mpango wa  uzazi.

Licha ya mimba za utotoni pia kumekuwepo na changamoto ya kutopanga uzazi hali ambayo imeelezwa kuwa  kwa mkoa wa Shinyanga uko nyuma kwa wanaotumia uzazi wa mpango ni asilimia 12.5  huku vifo vitokanavyo na uzazi ni asilimia 80 sababu ikielezwa ni  mama mjamzito kuchelewa kufika katika kituo cha afya  na wasichana kuzaa umri mdogo.


Hayo yalisemwa   na mganga mkuu wa mkoa  dkt  Ntuli Kapologwe  kwenye  ufunguzi  wa  semina ya uzazi wa mpango kwa waandishi wa habari wa kanda ya Ziwa na magharibi kwa mikoa ya  Simiyu,Tabora Mwanza, Kigoma ,Geita,Kagera ,Mara na Shinyanga  yaliyofanyika  mjini Shinyanga  huku akisema kuwa  kufikia mwakani inatakiwa kutimiza malengo ya  asilimia 60 na sasa ni asilimia 27 kitaifa.

“Vifo bado vipo vingi  sauti za waandishi wa habari zikitumika  zinaweza kupunguza changamoto iliyopo kwani   afya ya mama na  mtoto bado iko nyuma  sababu ya kushindwa kupanga uzazi  na kufikia asilimia 12.5  kwa mkoa wa Shinyanga  isipokuwa kwa suala la mtoto pekee limefanikiwa vizuri ambapo  jamii bado inawanyanyasa watoto wa kike kwa kuwaozesha mapema na kufanya ongezeko la  mimba za utotoni huku  viungo vyao vikiwa bado kukomaa.”alisema Dkt Kapologwe.

Mwezeshaji  Anna Mwalongo kutoka mkoani Shinyanga alisema kuwa  kuhusu masuala ya mpango wa uzazi   ni muhimu kuwapatia waandishi wa habari semina hii ili waweze kuripoti na kuleta mabadiliko chanya  ikiwa zaidi ya wanawake 8500  kitaifa hufariki  dunia  kwa matatizo yanayohusiana na uzazi.

Mwalongo alisema kuwa ongezeko la  watumiaji wa uzazi wa mpango ni asilimia 2.9 kila mwaka  ikiwa  wanawake 454 kati ya 100,000 hufariki  kwa mwaka,  na kati ya watoto 1000 watoto  51 wanafariki pia, kwa  wanaotumia  uzazi wa mpango kwa njia zote ni asilimia 34 huku aslimia 7 wakitumia njia za asili  pekee kupanga uzazi.

“Baadhi ya wanawake wamekuwa wakinunua  dawa za mpango wa uzazi kwenye maduka ya dawa ya watu binafsi,wasichana  wenye umri wa  uwezekano wa kupata mimba nao huwaibia wazazi wa o majumbani  hivyo takwimu zake zinashindwa kuhesabiwa kutokana na wenye maduka kutoorodhesha  idadi,pia kutofahamu ni wasichana wangapi wanatumia,ambapo asilimia 9.5 ya wanawake wanajikuta  wakipata watoto pasipo kutarajia wao huku wakilenga kupanga uzazi”alisema Mwalongo.

Naye mwakilishi kutoka wizara ya afya na ustawi wa jamii  kitengo cha afya ya uzazi na mtoto Zuhura  Mbuguni    alisema  kuwa  kuna baadhi ya vikwazo  ambavyo mwanaume kutomruhusu  mke wake  kutumia uzazi wa mpango ikiwemo kuishi mbali na vituo vya afya huku akisema suala la mpango wa uzazi sio kwa wanawake pekee  ni mke na mume au wapenzi.

Vikwazo vilivopo mke na mume au wenza kutojadiliana kuhusu idadi ya watoto wala kupanga uzazi, wanawake  kunyimwa uwezo wa kufanya maamuzi  kuhusu ngono,mimba na matumizi ya uzazi wa mpango,ukatili wa kijinsia  pamoja na ukeketaji huweza kuathiri utoaji huduma  na matumizi ya njia za uzazi wa mpango huku vijana walioanza kubalehe  wanakuwa na hofu kuonwa na watu  wakifuata huduma ya uzazi wampango”alisema Mwalongo.


0 Response to " UZAZI WA MPANGO MKOANI SHINYANGA WANAOTUMIA NI ASILIMIA 12.5 BADO KUNA CHANGAMOTO KUBWA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.