HIKI NI KISIMA KIREFU CHA MAJI AMBACHO WANANCHI WAKE HUPATA MAJI HAYO KWA KUPAMBU.
BAADHI ya wananchi wa
kijiji cha Bulekela kata ya Masanga wilayani Kishapu wameukataa
mradi wa maji uliotengewa jumla ya shilingi millioni 28.5 kwa madai ya kutoshirikishwa na wataalamu huku
wakitaka mabomba yasambazwe karibu na nyumba zao na sio visima
virefu au vifupi vya kupampu na mkono ambapo madiwani wameazimia kuondoa mradi
huo katika kijiji hicho.
Wananchi hao wameshauri
na mkuu wa wilaya Wilson Nkhambaku ,mkuu wa mkoa Ally Rufunga waupokee mradi huo kwa uwepo wake kwenye kijiji chao lakini bado wameonyesha
kutokubaliana nao na kudharau ushauri
huo kinachotakiwa ni kumtaka mkurugenzi kuhamisha mradi na kupeleka maeneo
mengine ambako wanashida ya maji.
Hayo yalibainishwa
kwenye kikao cha baraza la madiwani na baadhi ya madiwani wa halmashauri hiyo
huku diwani wa kata ya Masanga Shiboka Pombe akitoa kilio chake kwa
wananchi wa kijiji hicho, ambapo mradi wa maji wananchi wamekuwa
wakiukataa kutokana na sababu hizo pia kwa kupinga wataalamu walivyobaini
.
Diwani huyo
alisema kuwa zilitengwa jumla ya shilingi Mill 28.5 kwaajili
ya kuchimba visima virefu lakini maji yalipokosekana kwa mujibu wa
wataalamu akiwemo mhandisi wa maji Lucas Saidi waliamua
viwekwe visima vifupi viwili kwa fedha hizo kwa kijiji hicho
kimoja vitakavyotumia pampu ya mikono.
Pia diwani wa kata ya
Mwamashele Julius Kwihuja alisema
kuwa maazimio yalikuwa mradi huo uhamishwe kwani maeneo mengi wananchi wanateseka kwa
kukosa huduma ya maji wao wamepata kiburi kwanini wambembelezwe ikiwa hata kwenye kamati suala hili limezungumzwa kuwa mradi huo
uhamishwe wanajivunia kuwa karibu na mto.
“Wananchi wa kijiji cha
Bulekela wamekataa mradi wa maji,ikiwa
mkuu wa wilaya,mkoa wameenda kuwashauri
lakini bado wanakataa kwanini mradi huo usihamishwe wakati maeneo mengi hayana huduma ya
maji wamekuwa na kiburi sababu ya kuwa
karibu na mto hivyo kwanini pia tuwabembeleze hata kwenye kamati tumekwishalizungumza kuwa mradi huo uhamishwe……”alisema diwani
Kwihuja.
Hata hivyo mwenyekiti
wa halmashauri hiyo Justine Sheka alisema kuwa utafiti uliopatikana
hapo kuwa eneo hilo maji ni kidogo ila eneo walilochimba kisima maji yapo
kwa wingi ila wao bado hawataki hata mradi ukihamishwa tayari kunahasara manunuzi ya pambu ni shilingi million saba,gharama
ya uchimbaji shilingi million 20 tayari zimekwisha tumika.
Pia mhandis wa maji
Saidi alisema kuwa walipopima eneo hilo walibaini maji ni kidogo kwa kutotosheleza mtandao wa
maji ya pomba kwa kitaalamu hivyo wakashauri kuwa kuwekwe visima
vifupi vya pambu ya mikono lakini wananchi walipoelezwa walikataa na kutaka
mabomba yatakayo sambaaa mpaka majumbani mwao.
Naye mkurugenzi wa
halmashauri hiyo Jane Mwitagurwa alisema
kuwa malalamiko yaliyopo dhidi ya
wananchi kuwa wakati wataalamu wanapima hawakushirikishwa na wataalamu,hivyo
mpango wa upimaji uanze upya kwa
kuwashirikisha ikiwa utaratibu wa kusambaza mabomba ufanyike,wanachokataa kingine ni ile shida ya
kupampu kwa mkono.
“Kuhamisha mradi huo
utaleta tena gharama kubwa hakuna
fedha kinachotakiwa ni kuondoa
mgogoro uliopo,mpango wa upimaji uanze upya kwa kuwashirikisha wananchi na usambazaji wa maji kwenye mambo ufanyike shida yao hawataki
visima hivyo ambavyo vya kupampu kwa mkono ndicho kilichobainika kwenye kijiji
hicho”alisema mkurugenzi Mwitagurwa. |
0 Response to "WANANCHI WA KIJIJI CHA BULEKELA KATA YA MASANGA WILAYANI KISHAPU MKOANI SHINYANGA WAMEKATAA MRADI WA MAJI WA VISIMA VYA KUPAMBU KWA MKONO WAKITAKA KUSAMBAZWA KWA MABOMBA KARIBU NA MAJUMBANI MWAO,MADIWANI WATOA AZIMIO MRADI HUO UHAMISHWE KIJIJINI HAPO NA KUPELEKWA SEHEMU NYINGINE."
Post a Comment