Habari za hivi Punde

AJALI MBAYA YA MABASI KUGONGANA NA KUUA ZAIDI YA 35 NA 80 KUJERUHIWA -BUTIAMA


 Kufuatia ajali mbaya iliyohusisha magari matatu wilayani Butiama mkoani Mara idadi ya watu waliopoteza maisha ni 38 hadi sasa huku majeruhi wakiwa ni 80.
Kwa mujibu wa mkuu wa wilaya ya Butiama  Anjelina Mabula aliyezungumza na TBC muda mfupi uliopita ajali hiyo amesema ajali hiyo imehusisha basi la AM Coach lenye namba za usajili  T736 AWJ likitoka Musoma kwenda Mwanza limegongana uso kwa uso na basi T677 CYC J4 Express likitoka Mwanza kwenda Tarime na gari jingine dogo aina ya Nissan Corola P332 KKT likitoka eneo la Sabasaba yote yalikutana kwenye mteremko yakitokea juu kwenda Darajani katika kupishana hawakuweza kupishana yakagongana na wakati huo gari dogo likapaki pembeni nalo likagongwa kwa nyuma likasukumwa na kutumbukia mtoni.

Katika gari dogo kulikuwa na watu 8,wawili wamefariki dunia na majeruhi 36 kutoka kwenye mabasi nao wamefariki na majeruhi 80 wamekimbizwa katika hospitali ya mkoa wa Mara.

Madereva wote wamefariki dunia

0 Response to "AJALI MBAYA YA MABASI KUGONGANA NA KUUA ZAIDI YA 35 NA 80 KUJERUHIWA -BUTIAMA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.