Habari za hivi Punde

MASHAHIDI KESI ZA UKATILI,UBAKAJI WAMEKUWA HAWAJITOKEZI MAHAKAMANI NA KUISHA KINYEMELA.

KESI  ambazo zinazowakabili watuhumiwa wanaowafanyia ukatili watoto wadogo mkoani Shinyanga, zimedaiwa kukosa ushirikiano kwa upande wa mashahidi na kusababisha kesi hizo kufutwa bila ya watuhumiwa kuchukuliwa hatua yeyote ya kisheria.

Hayo yamebainishwa jana na Afisa wa ulinzi wa usalama wa mtoto Hermani Mmbunda, kutoka Shirika la Save the Children , linalofanya Shughuli zake mkoani Shinyanga, amesema asilimia kubwa ya kesi zinazopelekwa mahakamani juu ya ukatili kwa watoto wadogo zimekuwa hazifiki hadi mwisho kutokana na mashahidi kushindwa kutoa ushirikiano wakutosha.

Mmbunda amesema Shirika lao limekuwa likisaidia jamii inayotendewa vitendo hivyo, katika hatua ya awali hadi ngazi ya mahakama, lakini linapofika suala la ushahidi wa mtu aliyeshuhudia tendo hilo,wamekuwa hawahudhulii mahakani na wengine kukana hawajui chochote juu ya tukio hilo.

‘’katika kesi hizi za ukatili dhidi ya watoto, asilimia kubwa zimekuwa zikiisha kinyemela kutokana na kukosa ushahidi wa kutosha mahakani, ambapo mashahidi wa kesi hizi,wamekuwa hawatoi ushirikiano wa kutosha na wengine wakikana shitaka hilo” alisema Mmbunda na kuongeza kuwa.

“Tulipofanya utafiti juu ya suala hili la Mashahidi kutohudhuria na kukana matukio hayo,tuka baini kuwa asilimia kubwa ya watuhumiwa wa matukio hayo wanatoka ndani ya jamii husika (Ukoo), ambapo wamekuwa wakiitishana vikao vyao na kumaliza suala hilo kimyakimya na hivyo kupunguza nguvu ya kesi hiyo mahakamani”

Mmbunda alisema baadhi ya Mashahidi hao wamekuwa wakidai kutishiwa kutengwa na ukoo, huku wengine wakitishiwa maisha, na kuwafanya wakate tamaa ya kuendelea kutoa ushahidi mahakani dhidi ya kesi hizo za ukatili.

Amesema kufuatia matukio hayo Shrika hilo la Save the Children,limepanga mkakati kwa kushirikiana  na mashirika mengine yanayotetea haki za mtoto mjini humo,ikiwamo na  serikali, katika kuhakikisha wanatoa elimu ndani ya jamii kuanzia ngazi ya kata,vitongoji ,vijiji hadi wilaya.

Naye afisa ustawi wa jamii katika manispaa ya Shinyanga Emmanuel Nghabi, alisema katika matukio 100,ya ukatili dhidi ya watoto yaliyolipotiwa  mwaka jana (2013), kesi zilizopelekwa mahakamani na kutolewa ushahidi na watuhumiwa kufungwa jera ni kesi 27 tu kati ya Miamoja.

Nghabi alisema, kufuatia wananchi kushidwa kutoa ushahidi dhidi ya kesi hizo, huku wengine wakiwaficha watuhumiwa kumeendelea kuchangia kuwepo kwa matukio  ya kikatili dhidi ya watoto wadogo mkoani humo.

0 Response to "MASHAHIDI KESI ZA UKATILI,UBAKAJI WAMEKUWA HAWAJITOKEZI MAHAKAMANI NA KUISHA KINYEMELA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.